MADEREVA BODABODA WATAKIWA KUPEWA ELIMU YA UVAAJI WA KOFIA NGUMU


Na Ndalike/Kijukuu
KAHAMA.

Kutokana na ajali za pikipiki kuendea kujitokeza mara kwa mara Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA na kusababisha vifo na majeruhi,waendeshaji wa Pikipiki hasa vijana wametakiwa kupewa elimu ya uvaaji wa kofia ngumu, (helement) ikiwemo kufuata sheria za usalama barabarani.

Hayo yamesemwa na Mkazi wa Bukondamoyo, PANKARASI ITALUMA kwenye mazishi ya mtoto wake LUCAS ITALUMA (30) aliyefariki dunia jana kutokana na ajali pikipiki iliyotokea mwanzoni mwa mwezi wa tano mwaka huu.

Italuma amsema elimu itolewe kwa makundi yote huku akiwataka waendesha pikipiki kuzingatia sheria za usalama barabarani zilizotolewa na jeshi la polisi ili kuepusha ajali zinazoweza kusababisha vifo na majeruhi.

Naye Katekista wa kanisa katoliki kigango cha mtakatifu veronika Bukondamoyo ELADIUS PASCHAL ameitaka jamii kutambua kuwa maisha ya dunia ni mafupi hivyo ni vyema kutenda matendo mema ikiwamo kuwasaidia watu wenye uhitaji.

Wiki iliyopita aliyekuwa mfanyakazi wa idara ya maji na usafi wa mazingira mjini Kahama KUWASA, alifariki dunia kwa ajali ya pikipiki baada ya kuaanguka akiwa katika mwendo kasi na kutovaa kofia ngumu.

Marehemu Lucas Italuma ambaye alikuwa Dereva na fundi wa Magari ameacha mke nawatoto watatu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive