MAJI YAWA KERO KWA WAKAZI WA BUKONDAMOYO KAHAMA


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Wakazi wa kitongoji cha Kisiwani mtaa wa Bukondamoyo kata ya Mhungula halmashauri ya Mji wa KAHAMA wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji hali ambayo inasababisha kufuata huduma hiyo umbali mrefu pamoja na kutumia maji yasiyo salama.

Kutokana na hali hiyo, wananchi wa kitongoji hicho wameamua kushirikia katika ujenzi wa gati la Maji ya ziwa Viktoria ili kujihakikishia upatikanaji katika eneo hilo.

Wakizungumza na jana kwenye kikao cha kujadilia ujenzi huo, baadhi ya wananchi wamepongeza hatua hiyo na kuwataka wananachi wengine kushirikia kikamilfu katika ujenzi huo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Bukondamoyo NASHON YOHANA amesema ujenzi wa gati katika kitongoji hicho unatarajia kuanza Ijumaa hii na zoezi la kuchimba mtaro litaanza jumatatu wiki ijayo na kwamba hilo litakuwa gati la tano katika mtaa huo.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive