KICHANGA CHAOKOTWA KIKIWA KIMEKUFA NYAKATO WILAYANI KAHAMA


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Mtoto mchanga wa kiume anayekadiriwa kuwa wa siku ameokotwa akiwa amefariki dunia kandokando ya karavati lililopo Mtaa wa Nyakato Kata ya NYASUBI jirani na kituo cha Mafuta cha Front oil Mjini KAHAMA na mwanamke ambaye hajafahamika majina wala makazi yake.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Kichanga hicho ambacho kinasadikiwa kimetupwa tangu majira ya asubuhi kimeokotwa majira ya saa tisa alasiri.

Wakizungumza na KAHAMA FM, mashuhuda hao wamesikitishwa na kitendo hicho huku wakiomba hatua kali zichukuliwe dhidi ya mwanamke atakayebainika kutenda unyama huo.

Diwani wa Kata ya Nyasubi, ABEL SHIJA ameiomba jamii kutoa ushirikiano kwa viongozi wa serikali na jeshi la Polisi ambao wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo na na kusema kwamba kitendo cha kutupa mtoto hakina tija kwa jamii.

Jeshi la Polisi wilayani Kahama limefika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa kichanga hicho kwaajili ya kwenda kuuhifadhi kwenye chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Mji wa Kahama pamoja na taratibu zingine.

Matukio ya kutelekeza na kutupa watoto katika wilaya ya Kahama yamekuwa yakijitokeza Mara kwa mara ambapo mapema mwezi huu, mtoto mchanga mwingine aliokotwa akiwa mzima katika shamba moja kijiji cha Sungamile kata ya Mwalugulu Halmashauri ya Msalala.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive