WAFANYABIASHARA WA MABINGWA MSALALA WASEMA ENEO LA SOKO SI RAFIKI KWA BIASHARA ZAO



Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Wafanyabiashara katika soko la Mabingwa Kata ya Bugarama Halmashauri ya MSALALA Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA wamesema eneo hilo si rafiki na biashara zao kutokana na kuwa mbali na makazi ya watu hivyo kuwasababishia hasara katika bidhaa zao.

Wakizungumza kwenye kipindi cha Raha ya leo, cha KAHAMA FM, wananchi hao wamesema tangu wahamishiwe katika soko hilo mwaka jana, wateja hawafiki kwa wingi kwani wananunua kwa wachuuzi wanaozungusha biashara katika makazi ya watu.

Mwenyekiti wa soko la hilo, SALOME HAMISI ameiomba halmashauri iboreshe miundombinu ya eneo hilo ikiwamo kuimarisha kituo kikuu cha mabasi cha Halmashauri hiyo na vivutio vingine.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Bugarama PRISCA PIUS amesema uongozi wa kata hiyo umekusudia kufungua mnada wa mifugo na mazao katika eneo hilo huku diwani wa viti maalum wa kata hiyo, PRISCA MSOMA amesema ni ufinyu wa bajeti na kwamba wanakusudia kuwarejesha soko la zamani.

Eneo la soko la Mabingwa lipo katika eneo la kituo kikuu cha mabasi cha halmashauri ya Msalala, ambapo tangu kufunguliwa kwake mwaka jana, mabasi yamekuwa hayaegeshi eneo hilo hivyo kusababisha wafanyabiashara waliohamishiwa eneo hilo kuendelea kulalamika.
Share:

2 comments:

  1. DUUUUUUUUUUUU!!!!!!!!!! INATAKIWA WAPEWE ENEO MAALUUUM

    ReplyDelete
  2. SERIKALI ILIANGALIE KATIKA JICHO LA KIMAISHA YA KIAFYA HASA MAZINGIRA NA UTUNZAJI WA CHAKULA

    ReplyDelete

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive