MIMBA NA NDOA ZA UTOTONI CHANGAMOTO KWA WANAFUNZI WILAYANI KAHAMA


Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Kukosekana kwa Elimu juu ya Masuala ya ndoa na mimba za Utotoni kwenye jamii Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA kunawanyima haki ya kupata elimu Wanafunzi chini ya miaka 18 kutokana na baadhi yao kupata ujauzito.

Hayo yamebainishwa na Afisa Ustawi wa Jamii wa Halmashauri ya Mji wa Kahama, ABDURAHMAN NURU wakati akitoa elimu juu ya kupambana na ndoa na mimba za utotoni kwa wazazi katika kata ya Iyenze.

NURU ametahadharisha kwamba ikiwa wazazi hawataacha kuwaozesha watoto wa kike husasani wanafunzi kwa tamaa ya kupata mali watakabiliwa na mkono wa sheria.

Naye Meneja Mradi wa kuzuia ndoa na mimba za utotoni kwa watoto chini ya miaka 18 kutoka shirika lisilo la kiserikali la Rafiki - SDO, ELIUD LAZARO amesema wameamua kutoa elimu hiyo kwa wazazi ili waweze kutoa malezi bora kwa watoto wao.

Kwa upande wake KERILIAN DANFORD ambaye ni miongoni mwa watoto wa kike waliofanikiwa kupata elimu hadi chuo kikuu na sasa ameajiriwa na Shirika hilo la Rafiki – SDO, amewaomba wazazi kuwasomesha watoto wakike ili waweze kutimiza ndoto zao za maisha.

Mkoa wa Shinyanga unaongoza kwa tatizo la ndoa na mimba za utotoni hapa nchiniuikifuatiwa na mikoa ya Geita,Tabora na Simiyu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive