WAZAZI WENYE WATOTO ALBINO WAASWA KUTOWAFICHA


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Wazazi na walezi wenye watoto wenye ualbino wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA imetakiwa kutowaficha watoto wao badala yake wawape haki zao za msingi ikiwamo matibabu na elimu bila usiri wowote.

Hayo yameelezwa leo na afisa tatibu wa hospitali ya Mji wa Kahama Dkt. FLORA MWINUKA kwenye kipindi cha raha ya leo kinachorushwa na Kahama fm ambapo amesema bado kuna baadhi ya wazazi wanawaficha watoto wao wenye ualbino licha ya elimu kuendelea kutolewa.

Amesema changamoto hiyo imekuwa ikisababisha unyanyapaa, na kuwanyima haki zao za msingi kama watoto wengine na kwamba jamii iache imani potovu dhidi ya watu wenye ualbino.

Kwa upande wake Katibu wa chama cha watu wenye ualbino Tanzania (TAS) Wilaya ya Kahama SITA MASENYA amesema chama hicho kimekuwa kikitoa elimu kwa jamii ili iwe tayari kuwapokea watu wenye ualbino.

Kwa mujibu wa MASENYA kwa sasa jamii wilayani Kahama imekuwa na uelewa dhidi ya watu wenye ualbino hali ambayo imepunguza matukio ya unyanyapaa na ukatili dhidi ya watu hao katika miaka ya hivi kaaribuni.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive