WAWILI WAINGIA PORI LA AKIBA LA KIGOSI MOYOWOSI BILA KIBALI NA KUKUTWA NA SILAHA



Na Daniel Magwina
KAHAMA.

Wakazi wawili wa kijiji cha Kalenga Wilayani Biharamulo, Mkoani Kagera, SIYAJALI KALOLI (37) na ELIAS DOTTO (20) wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya kuingia katika Pori la Akiba la Moyowosi - Kigosi na kupatikana na silaha bila kibali.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo KENETH MUTEMBEI, mwendesha mashitaka wa Idara ya wanyamapori, INNOCENTI MUTAGWABA amesema Mei 2O mwaka huu saa mbili usiku Washitakiwa waliingia ndani ya Pori hilo bila kibali cha Mkurugenzi wa Wanyamapori.

MUTAGWABA amesema washitakiwa hao pia walikamatwa wakiwa na msumeno ambao walikuwa wanautumia kukatia miti ya kupasulia mbao kinyume cha sheria.

Washitakiwa wote wamekiri kutenda makosa yote mawili kuingia hifadhi bila kibali pamoja na kupatikana na msemeno katika hifadhi kinyume cha sheria

Katika shitaka la pili washitakiwa wanadaiwa kupatikana na silaha kinyume na kifungu namba103 cha sheria ya uhifadhi Wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009.

Katika shauri hilo la jinai naimba 190/2018 washitakiwa wametenda kosa la kwanza la kuingia hifadhi bila kibali kinyume na kifungu namba 18 cha sheria ya wanyamapori namba 5 ya mwaka 2009.

Washitakiwa wote wamerudishwa rumande kwa kukosa dhamana hadi shauri hilo litakapo tajwa tena mahakamani hapo Juni 6 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive