WAUMINI WA DINI YA KIISLAM WILAYANI KAHAMA WAASWA KUTUMIA MWEZI MTUKUFU KUKEMEA MAOVU


Na Ndalike Sonda
KAHAMA.

Waumini wa dini ya Kiislamu Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA wameaswa kuutumia mwezi Mtukufu wa Ramadhan kukemea matendo maovu ambayo yamekuwa yakijitokeza katika jamii hasa mauaji ya vikongwe pamoja na kuzingatia swala.

Wito huo umetolewa na Shekhe wa Wilaya ya KAHAMA, OMARY DAMKA wakati akizungumza kwenye kipindi cha raha ya leo cha KAHAMA FM kuhusu Mfungo wa Ramadhani ulioanza leo ambapo amesema Waisilam wanapaswa kutenda yaliyo mema ili kupata thawabu.

Aidha SHEKHE DAMKA amewaasa wafanyabiashara wilayani humo kutopandisha bei za bidhaa mbalimbali wakati wa mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan badala yake wauze kwa bei ya kwaida ili kuwawezesha Waumini kumudu gharama ya bidhaa zinazohitajika wakati huu wa mfungo.

Mmoja wa waumini wa dini hiyo na mkazi wa Kijiji cha Sangilwa, halmashauri ya mji wa Kahama, SAID HAMAD amesema mwezi Mtukufu wa Ramadhan utawasaidia kuwakumbusha maagizo ya Mtume Muhamad kwa Waisalam wote.

Mwezi mtukufu wa Ramadhan ni nguzo ya nne katika nguzo tano za Uisilam ambapo mwezi huu Waislam ulimwenguni kote huutumia kufunga kwa toba na kufanya mema.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive