MFANYAKAZI WA KUWASA KAHAMA AFARIKI KWA AJALI YA PIKIPIKI



Na Daniel Magwina
KAHAMA.

Mkazi wa Nyahanga Mjini KAHAMA na mfanyakazi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mjini Kahama mkoani shinyanga, REXPIRIUS VICENT (29) amefariki dunia kwa ajali ya pikipiki iliyotokea mapema leo alfajiri katika mtaa wa Igalilimi mjini humo.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo mkuu wa kitengo cha usalama barabarani wilayani Kahama DESIDERI KAIGWA amesema kuwa ajali hiyo imehusisha pipipiki aina ya boksa yenye namba za usajili T (40403), aliyokuwa akiendesha Marehemu VICENT.

KAIGWA amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva pamoja na kutokuvaa kofia ngumu na ametoa rai kwa watumiaji wa vyombo vya moto hususani pikipiki kuvaa kofia ngumu ili kuchukua tahadhari pindi ajali inapotokea.

Msemaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira mji Kahama (KUWASA), JOHN MKAMA pamoja na kueleza jinsi walivyopokea taarifa ya msiba huo amesema taratibu za mazishi zinaendelea kufanyika na kwamba mwili wa marehemu utasafirishwa kuelekea kwao mkoani Kigoma kwa ajili ya mazishi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive