WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI MANISPAA YA SHINYANGA WATAKIWA KUPAMBANA NA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA ILI KUTIKOMEZA VITENDO HIVYO KWENYE JAMII



Na Salvatory Ntandu
KAHAMA.

Walimu wa shule za Msingi na sekondari katika manispaa ya SHINYANGA wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi ili kutokomeza vitendo hivyo kwenye jamii.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya SHINYANGA, JOSEPHINE MATIRO wakati akifungua warsha maalumu kwa walimu wa Manispaa hiyo yenye lengo la kuwajengea uelewa kuhusu masuala ya jinsia iliyoandaliwa na chuo kikuu huria Tanzania.

Amesema mbinu stahiki za kupambana na ukatili wa kijinsia zitafanikiwa endapo dhana, aina, matokeo na sababu za ukatili zitaeleweka kuanzia ngazi ya msingi hususani shuleni ambapo watoto wanatumia muda mwingi wa maisha yao.

MATIRO amefafanua kuwa walimu hukaa na wanafunzi kwa muda mrefu hivyo wanapaswa kuzijua athari zinazowakumba wanafunzi pindi wanapofanyiwa vitendo hivyo na namna vinyowaathiri kitaaluma.

Mbali na hilo MATIRO amewataka walimu kuweka kanuni na taratibu ambazo zitatoa ulinzi na kusaidia jamii nzima ya shule kuishi kwa amani na kuzingatia usawa ili wanafunzi wawezekufanya vizuri katika mitihani yao.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Kituo cha Shinyanga, PASCHAL MHELUKA amesema lengo la warsha hiyo ni kuwajengea uelewa walimu kuhusu masuala ya jinsia ili wakawafundishe wanafunzi ambao watakuwa mabalozi katika jamii.

Amebainisha kuwa kwa sasa wamewafikia walimu 100 kutoka shule za msingi na sekondari za serikali na binafsi wanaofundisha somo la uraia kwani wanafundisha masuala mtambuka yanayohusu mambo ya jinsia.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive