
Rais John Magufuli ametuma salamu za rambirambi na pole kutokana na ajali ya kivuko cha Mv Nyerere kilichozama jana mchana Septemba 20,2018 huku watu 44 mpaka sasa wakiripotiwa kufariki dunia.
Kivuko hicho kilikuwa kinatoka Bugorora kwenda Ukara katika Ziwa Victoria kilizama kikidaiwa kuwa na watu zaidi ya 100.
Rais
 Magufuli ametoa salamu hizo  jana usiku saa 20:40   kupitia kwa 
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Gerson Msigwa aliyepiga simu 
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wakati wa taarifa ya habari.
“Rais anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki waliofikwa na ajali,” alisema Msigwa
Msigwa
 alisema, “Rais anaomba Watanzania kuwa watulivu wakati juhudi za 
uokoaji zinaendelea na baadaye Serikali itaweza kutoa taarifa ya nini 
kitakachoendelea.”






No comments:
Post a Comment