Jeshi
 la Polisi mkoani hapa limefanikiwa kupata gari lililoibiwa aina ya 
Toyota Surf lenye namba za usajili T.996 AGK pamoja na Bastola aina ya 
Browning iliyokuwa na risasi Nane ndani ya Magazine. 
Akizungumza
 na Waandishi wa habari jana mchana  Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha
 Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi alisema
 kwamba tukio la kuibiwa kwa gari hilo lililokuwa linaendeshwa na Bi. 
Sarah Cornel (40) Mwalimu wa Sekondari na ni mkazi wa Olasiti jijini 
hapa lilitokea Septemba 17 muda wa saa 9:50 Alasiri katika maeneo ya 
Stand Ndogo.
“Mara
 baada ya kuegesha gari lake maeneo ya Stendi Ndogo alienda madukani kwa
 ajili ya kufanya manunuzi aliporudi hakulikuta ndipo alipoelekea kituo 
Kikuu cha Polisi kwa ajili ya kutoa taarifa ambayo ilifanyiwa kazi kwa 
kuanza kuweka vizuizi maeneo ya barabara kuu na kufanya msako mkali”.
Alisema
 wahalifu hao baada ya kuona njia zote zimedhibitiwa waliamua 
kulitelekeza gari hilo katika kituo cha Afya Kaloleni kilichopo jijini 
hapa ambapo siku ya pili muda saa 05:30 Asubuhi lilipatikana huku 
watuhumiwa wakiwa wametoweka na Jeshi hilo linaendelea kufanya uchunguzi
 wa Kisayansi ili kuweza kuwabaini.
Mbali
 na tukio hilo Polisi mkoani hapa wameweza kupata silaha aina ya bastola
 ambayo ilikuwa na risasi nane ndani ya Magazine, Kamanda Ng’anzi 
alisema lilitokea Septemba 15 mwaka huu katika kijiji cha Kimyaki 
kilichopo tarafa ya Enaboishu wilayani Arumeru.
Alisema
 Jeshi hilo lilipata taarifa hiyo toka kwa raia wema ambapo waliwadokeza
 kuwapo kwa silaha hiyo ndani ya chumba cha mtu waliyekuwa wanamdhania 
mhalifu ndipo askari walikwenda katika eneo hilo na kufanikikwa kupata 
silaha hiyo ambayo wanakiri ilikuwa inamilikiwa isivyo halali na Jeshi 
hilo linaendelea na msako mkali kumtafuta mtuhumiwa huyo.
Mbali
 na mafanikio hayo msako wa Jeshi hilo umeweza kufanikisha kupata mali 
mbalimbali zikiwemo TV mbili “flat Screen”, Laptop, Jenereta na vitu 
vingine ambavyo vinasadikiwa kuibiwa katika mitaa mbalimbali ya jiji la 
Arusha siku za nyuma.
Kwa
 upamde wa Usalama barabarani Jeshi hilo limepanga kuanzisha kikosi 
maalum kwa ajili ya kuwadhibiti waendesha boda boda wanaovunja sheria 
hasa za kubeba abiria zaidi ya mmoja maarufu kama “Mishikashi” na wale 
wanaovuka mataa bila kuruhusiwa.
Kamanda
 Ng’anzi alisema kikosi hicho kitakuwa na askari ambao watakuwa wanavaa 
kiraia na watasambazwa katika maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha hali 
ambayo anaamini itakomesha tabia ya madereva wa boda boda wanaovunja 
sheria kwa makusudi.






No comments:
Post a Comment