AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA UNYANG'ANYI


Na Lilian/Paulina
KAHAMA.

Mkazi wa Mkoa wa Geita CLEMENT KAYANDA (24) amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya unyang’anyi kwa kutumia Silaha aina ya rungu pamoja na panga kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo KENETH MUTEMBEI, mwendesha mashitaka wa Polisi PETER MASAU amesema May 5 mwaka huu majira ya saa 10 usiku huko kijiji cha Ilogi, KAYANDA aliiba kaboni gram 300 za kuchenjua dhahabu zenye thamani ya shilingi milioni arubaini mali ya DIANA JILUMBA.

MASAU amesema KAYANDA ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 287 A cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

Katika shauri hilo la jinai namba 184/2018 KAYANDA amekana kutenda kosa hilo na amerudishwa rumande kwa kuwa kosa analotuhumiwa halina dhamana na shauri hilo litatajwa tena May 31 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive