Mwanafunzi
 wa kike (15) aliyekuwa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Nsemlwa, 
Manispaa ya Mpanda, mkoani Katavi amenusurika kujiua kwa kujinyonga 
baada ya baba yake Bushiri Joseph, kumuwahi akiwa tayari amepanda juu ya
 kiti baada ya kulazimishwa kuendelea na masomo.
Mwanafunzi
 huyo pamoja mwenzake wa kiume mwenye umri wa miaka 16, anayesoma kidato
 cha pili katika shule hiyo, wanadaiwa kuwa watoro sugu na kutishia 
kujiua kwa kujinyonga kwa kamba au kunywa sumu iwapo wazazi na walimu 
wao wataendelea kuwalazimisha kuendelea na masomo.
Licha
 ya kuhojiwa na wazazi na walimu wao, wanafunzi hao hawakuwa tayari 
kueleza kinachowasababisha wakatae kuendelea na masomo na badala yake 
wamekuwa wakitishia kujiua kama watalazimishwa kurejea shuleni.
Inadaiwa kuwa wazazi wa wanafunzi hao wameshawafikisha kituo cha polisi bila mafanikio, wakiwa na msimamo wao wa kujiua.
Mwalimu
 Mkuu wa shule hiyo, Edgar Mwaisunga, aliwaambia waandishi wa habari 
kuwa mwanafunzi huyo alifikishwa na baba yake mzazi shuleni hapo 
kujiunga na kidato cha kwanza Januari, mwaka huu.
"Baba
 yake alikuwa amemnunulia kila kitu alichohitaji binti yake, lakini 
miezi miwili baadaye alianza utoro, tukimhoji alikuwa akidai kuwa hataki
 kuendelea na masomo...tulidhani kuwa ni mjamzito, lakini alipopimwa 
hakuwa na ujauzito,” alisema.
Alisema
 walimu walijitahidi kumsihi, lakini msichana huyo alikataa kata kata 
kuendelea na masomo...lakini alikuwa haelezi kwanini hataki kuendelea na
 masomo, huku akitishia kujiua kama atalazimishwa kuendelea na masomo," 
alisema.
Kwa
 mujibu wa Katibu wa Baraza la Kata ya Uwanja wa Ndege, Manispaa ya 
Mpanda, Salum Msimani, wanafunzi hao wawili ni miongoni mwa 17 wa Shule 
ya Sekondari Kasimba, Manispaa ya Mpanda, waliofikishwa katika Baraza la
 Kata na kufunguliwa mashtaka ya utoro shuleni.
"Wanafunzi
 hao msichana na mvulana waliokuwa wakisoma katika Shule ya Sekondari 
Nsemlwa, wakiwa na wazazi na walezi wao walifikishwa wiki iliyopita 
kwenye Baraza la Kata la Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Mpanda na kusomewa
 mashtaka yao baada ya mkuu wao wa shule na bodi ya shule hiyo 
kuwasilisha malalamiko dhidi yao na wazazi wao kwenye baraza hilo," 
alieleza Msimani.
Msimami
 alisema wanafunzi hao wakiwa kwenye baraza hilo waliendelea na msimamo 
wao wa kukataa kuendelea na masomo, huku wakisisitiza kuwa kama 
watalazimishwa kuendelea na masomo watajiua kwa kujinyonga kwa kamba au 
kunywa sumu .
Alisema, walipotakiwa kueleza sababu zinazowafanya wakatae kuendelea na masomo hawakuwa tayari kuzieleza.
"Baraza
 hili limeshindwa kutoa hukumu dhidi ya wanafunzi hawa wawili na hata 
shuleni walikokuwa wanasoma walimu wameinua mikono, pia polisi 
wamefikishwa na wazazi wao, lakini imeshindikana wameng'ang'ania msimamo
 wao,” alisema na kuongeza:
“Kama
 Katibu wa Baraza hili la Kata natarajia kuonana na Hakimu wa Mahakama 
ya Wilaya ya Mpanda kwa ushauri wa kisheria," alisisitiza.
Aidha,
 alieleza kuwa kamba aliyotaka kujinyongea mwanafunzi wa kike na kiti 
alichokuwa amepanda, vipo katika ofisi za baraza hilo.
Baba
 mzazi wa mwanafunzi huyo wa kike, Bashir Joseph, amedai kuwa hivi 
karibuni alipomlazimisha binti yake kwenda shuleni aligoma na kuingia 
chumbani kwake alikokuwa ametundika kamba ya kujinyongea na kumkuta 
akiwa amepanda kwenye kiti tayari kwa kujinyonga.
Naye
 baba mzazi wa mwanafunzi wa kiume, Sadok Isha, amedai kuwa pamoja 
kuchukua hatua mbalimbali za kumfanya kijana wake huyo aendelee na 
masomo, lakini imeshindikana baada ya kutishia kujinyonga.
Diwani
 wa Kata ya Uwanja wa Ndege, Stephano Asalile, alisema kwa tukio la 
wanafunzi hao wawili linaonyesha jinsi ambavyo baadhi ya wazazi wa 
wanafunzi wamekuwa wakipewa adhabu kutokana na utoro wa watoto wao, 
kumbe tatizo lipo kwa watoto wenyewe.






No comments:
Post a Comment