Benki
 Kuu ya Tanzania imeongeza muda wa usimamizi wa Bank M Tanzania Plc 
(Bank M) kwa siku 60 zaidi kuanzia tarehe 2 Novemba 2018.
Kwa
 mamlaka iliyopewa chini ya kifungu namba 56 (1) (g) (iii) cha Sheria ya
 Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006, Benki Kuu ya Tanzania 
ilichukua usimamizi wa Bank M kuanzia tarehe 2 Agosti 2018 baada ya 
kubaini kuwa benki hiyo ilikuwa na upungufu mkubwa wa ukwasi kinyume na 
matakwa ya sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006 na kanuni
 zake.
Baada
 ya kuchukua usimamizi, Benki Kuu ya Tanzania ilisitisha shughuli za 
utoaji wa huduma za kibenki za Bank M kwa muda wa siku tisini (90) ili 
kuipa nafasi Benki Kuu ya Tanzania kutathmini hatua za kuchukua ili 
kupata ufumbuzi wa suala hilo.
“Benki
 Kuu ya Tanzania inapenda kuuarifu umma kuwa mchakato wa kutathmini 
hatua za kuchukua ili kupata ufumbuzi wa matatizo ya Bank M 
haujakamilika; hivyo muda wa usimamizi umeongezwa kwa kipindi cha siku 
60 kuanzia tarehe 2 Novemba 2018,” kwa mujibu wa taarifa kwa umma 
iliyotolewa leo.
Aidha,
 Benki Kuu ya Tanzania inauhakikishia umma kuwa itaendelea kulinda 
maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta ustahimilivu 
katika sekta ya fedha.
 






No comments:
Post a Comment