Serikali imeendelea kuchukua hatua za kubatilisha milki za ardhi za mashamba yaliyotekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Hayo
 yamesema Bungeni jana na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya 
Makazi Angelina Mabula  wakati akijibu swali la Mhe. Dustan Kitandula 
Mbunge wa Mkinga kuhusu kufuta hati za mashamba yaliyotelekezwa.
“Katika
 kipindi cha Disemba, 2015 mpaka Octoba, 2018 mashamba yenye ukubwa wa 
ekari 84,240.803 yamebatilishwa katika Halmashauri za Ngorongoro, 
Arumeru, Moshi, Kinondoni,(Manispaa), Kigamboni(Manispaa), Mvomero, 
Kilombero, Kilosa, Mvomero, Iringa, Bukoba, Tarime, Kibaha, Serengeti, 
Busega, Muheza, Lushoto na Mkinga” amefafanua Naibu Waziri Mabula.
Mabula
 anasema kuwa, katika Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, Shamba Na. 278 
Mkomazi lenye ukubwa wa ekari 15,442 lililokuwa likimilikiwa na kampuni 
ya M/S Mkomazi Plantations Limited kwa Hati Namba 4268, 9780  na 9781 
milki yake ilithibitishwa tarehe 20 Juni, 2018.
Aidha
 anafafanua kuwa, baada ya kubatilishwa kwa milki ya shamba hilo, 
Serikali ya Mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya 
Mkinga zipange matumizi mapya ya shamba hilo kwa kuzingatia mahitaji ya 
ardhi katika eneo hilo kipaumbele kikiwa ni mahitaji ya wananchi na 
ardhi kwa ajili ya uwekezaji.
Mbali
 na hayo Mabula amezitaka Halmashauri zote nchini kubaini mashamba 
yaliyotelekezwa kutuma ilani kwa wamiliki wa mashamba hayo kwa mujibu wa
 Sheria ya Ardhi (Sura 113) na kuwasilisha mapendekezo katika Wizara ya 
Ardhi kwa hatua za kubatilisha milki za mashamba hayo ziweze kufanyika.






No comments:
Post a Comment