WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigela orodha ya matrafiki wanaodaiwa kuwaomba rushwa madereva wa noah wilayani Lushoto.
Majina
 ya trafiki hao wanadaiwa kuomba rushwa kwa madereva wa noah wanaofanya 
kazi ya kusafirisha abiria ndani ya wilaya hiyo yaliwasilishwa kwa 
Waziri Mkuu kupitia mabango.
Waziri
 Mkuu alimkabidhi majina hayo jana jioni (Jumatano, Oktoba 31, 2018) 
baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara katika uwanja wa 
Sabasaba, Lushoto mjini.
Baada
 ya kumkabidhi majina hayo alimuagiza afanye uchunguzi wa tuhuma za 
rushwa zinazowakabili askari hao na kisha awasilishe taarifa kwake leo 
Alhamisi Novemba 1, 2018.
Mbali
 ya wananchi kuwasilisha malalamiko hayo, Pia mbunge wa Lushoto, Shaaban
 Shekilindi alimuomba Waziri Mkuu awasaidie kutatua kero hiyo 
inayowakabili wananchi.
Awali,
 Waziri Mkuu alizungumza na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya 
Lushoto katika ukumbi wa chuo cha Mahakama Lushoto ambapo aliwasisitiza 
wafanye kazi kwa bidii.
Alisema
 Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli haina
 msamaha na mtumishi wa umma asiyetaka kufanya kazi kwa bidii na 
kuzingatia weledi.
Alisema
 watumishi wa umma wanatakiwa kufanya kazi kwa kufuata maadili ya 
utumishi ili waweze kutimiza lengo la Serikali la kuwahudumia wananchi 
kwa kutumia taaluma zao.
Waziri
 Mkuu ambaye alikuwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi mkoani 
Tanga alisema Serikali haina msamaha na mtumishi asietaka kubadilika na 
kufanya kazi.
Pia,
 Waziri Mkuu aliwataka watumishi wa umma wahakikishe fedha zinazotolewa 
na Serikali kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo 
zinatumika kama ilivyokusudiwa.
Kadhalika,
 Waziri Mkuu aliwataka Wakuu wa Idara kutumia kitabu cha ilani ya 
uchaguzi cha CCM cha mwaka 2015/2020 kwa sababu kina maelekezo 
wanayopaswa kuyatekeleza.
“Kitabu
 kile kina maelezo ya msingi yaliyotolewa na Rais. Dkt. Magufuli ambayo 
yanatakiwa yapewe kipaumbele cha utekelezwaji, wakuu wa Idara ni muhimu 
musome na kutekeleza.”
Waziri
 Mkuu alitumia fursa hiyo kuwataka wakuu wa wilaya wahakikishe 
wanasimamia utekelezwaji wa maelekezo yote yaliyoainishwa kwenye kitabu 
cha Ilani katika maeneo yao.
Kuhusu
 changamoto ya upungufu wa watumishi wa kada mbalimbali nchini, Waziri 
Mkuu alisema Serikali inatambua na kwamba suala hilo linaendelea 
kufanyiwa kazi.
Katika
 hatua nyingine, Waziri Mkuu alizungumza na wananchi katika mkutano wa 
hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba na kuwapongeza wakazi hao 
kwa kutunza misitu.
Alisema
 maeneo mengi nchini wananchi wamekata miti na kusababisha kukauka kwa 
vyanzo vya maji, ambapo ni tofauti na wilaya ya Lushoto ambayo bado ina 
misitu minene.
Kufuatia
 hali hiyo Waziri Mkuu aliwaagiza watendaji wote wa vijiji na kata 
waainishe sehemu  zote zenye misitu na vyanzo vya maji katika maeneo yao
 na wahakikishe wanayalinda.
Alisema
 mtu yeyote atakayebainika kuharibu mazingira hayo iwe kwa kuchoma au 
kukata miti achukulie hatua kali. “Ni marufuku mtu yeyote kukata miti 
bila kibali cha Serikali.”
Nae,
 Mbunge wa Lushoto Shekilindi alimuomba Waziri Mkuu awasaidie katika 
kuwatatulia changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa katika 
jimbo hilo ikiwemo ya afya.
Mbunge alisema kwa sasa hospitali ya wilaya hiyo inakabiliwa na ukosefu wa mashine ya x
rey, hivyo kusababisha wananchi kusafiri hadi Korogwe au Tanga kufuata huduama hiyo.
Waziri
 Mkuu alisema tayari ameshamuagiza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, 
Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kupeleka mashine ya x-rey katika 
hospitali hiyo.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, NOVEMBA 1, 2018.






No comments:
Post a Comment