Marekani imetangaza kuwa leo Nov 5 imeirejeshea vikwazo nchi ya Iran vitakavyolenga sekta ya mafuta na sekta ya kifedha.
Marekani imesema imeiwekea Iran vikwazo vigumu zaidi ambavyo haijawahi kuiwekea. Vikwazo hivyo vitalenga mauzo ya mafuta, usafiri kwa njia ya baharini na mabenki ambavyo vyote ni muhimu sana kwa uchumi.
Maelfu
 ya raia wa Iran wakiwa na mabango yaliyoandikwa  "Kifo kwa Marekani" 
wameandamana  wakiitaka serikali  yao kutofanya mazungumzo yoyote na 
Marekani.
Jeshi la Iran nalo limesema kuwa litafanya mazoezi ya kijeshi leo Jumatatu na Jumanne kuonyesha uwezo wake wa kijeshi.
Marekani
 imetangaza vikwazo hivyo  baada ya  Rais Trump kutangaza  kujitoa 
kwenye  mkataba wa mwaka 2015 uliolenga kupunguza mipango ya nyuklia ya 
Iran.
Marekani
 inasema inataka kuzima vitendo viovu vya Ina vikiwemo udukuzi wa 
mitandao, majaribio ya makombora ya masafa marefu na uungaji mkono wa 
makundi ya kigaidi mashariki ya kati.
Zaidi
 ya watu 700, kampuni, vyombo vya habari na ndege kwa sasa vimewekewa 
vikwazo, yakiwemo mabenki makubwa, wauza mafuta na kampuni za usafiri wa
 baharini.
  
Wakati
 hayo yakijiri, Uingereza , Ujerumani na Ufaransa ambazo ni kati ya nchi
 zilizo kwenye makubaliano ya nyuklia zote zimekataa vikwazo hivyo vya 
Marekani dhidi ya Irani.
Zimeahidi
 kuzisaidia kampuni za Ulaya zinazofanya baishara halali na Iran na 
kubuni njia mbadala za malipo ambazo zitasaidia kampuni kufanya bishara 
bila ya vikwazo vya Marekani






No comments:
Post a Comment