Kikosi
 cha timu ya Taifa ya Tanzania "Taifa Stars"  kimeondoka alfajiri ya 
jana kwenda Afrika Kusini kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo dhidi ya 
Lesotho katikati ya mwezi huu kwa ajili ya kufuzu Fainali za Kombe la 
Mataifa ya Afrika (AFCON) mwakani, nchini Cameroon.
Kikosi
 hicho kimeondoka kikiwa na matumaini makubwa kwamba mazoezi 
watakayoyafanya yatawasaidia kuibuka na ushindi mchezo wao ujao dhidi ya
 Lesotho ugenini.
Taifa
 Stars watakuwa wageni wa Mamba wa Lesotho Novemba 18, mwaka huu, Uwanja
 wa Setsoto mjini Maseru, katika mchezo wa Kundi L kufuzu AFCON ya 
mwakani, itakayofanyika Cameroon.
Kikosi
 hicho kitaweka kambi ya siku 10 nchini Afrika Kusini kikijifua vikali 
chini ya Kocha wake Mkuu, Mnigeria Emmanuel Amunike na msaidizi wake, 
Hemed Morocco.
Wachezaji
 waliosafiri na Stars ni pamoja na makipa Aishi Manula wa Simba SC, 
Aaron Kalambo wa Tanzania Prisons, Beno Kakolanya wa Yanga SC na 
Benedictor Tinocco wa Mtibwa Sugar.
Mabeki
 ni Shomary Kapombe, Erasto Nyoni wa Simba SC, Ally ëSonsoí Abdulkarim 
wa Lipuli FC, Kelvin Yondan, Gardiel Michael wa Yanga SC, Aggrey Morris 
na Abdallah Kheri wa Azam FC.
Viungo
 ni Salum Abubakar ëSure Boyí, Mudathir Yahya wa Azam FC, Salum Kimenya 
wa Tanzania Prisons, Feisal Salum wa Yanga SC, Jonas Mkude na Shiza 
Kichuya wa Simba SC.
Washambuliaji
 ni Thomas Ulimwengu aliye huru baada ya kuvunja mkataba na Al Hilal ya 
Sudan mwishoni mwa wiki, John Bocco wa Simba SC na Yahya Zayed wa Azam 
FC.






No comments:
Post a Comment