Sakata la kukamatwa kwa Mbunge wa Kigoma mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe na kushindwa kupatiwa dhamana jana Oktoba 31, kumemuibua kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni Freeman Mbowe na kudai kuwa wabunge waupinzani waachwe wafanye kazi yao.
Mbowe
 ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA taifa, amefunguka hayo kupitia 
ukurasa wake wa kijamii wa twitter ambapo ameandika kuwa, "Mhe Zitto 
kasema na Vyombo vya Ulinzi na Usalama vimehusishwa. Wanasiasa wa 
Upinzani waachwe wafanye kazi yao, mtuhumiwa asiwe Hakimu. Serikali 
ijibu hoja kwa vielelezo, ikilazimu iunde tume huru za uchunguzi na 
CHADEMA tutasimama na ACT".
Zitto
 alikamatwa na polisi jana saa 5 asubuhi na kupelekwa kituo cha polisi 
Oysterbay ambako alihojiwa kwa takribani saa tatu, kisha kuhamishiwa 
kituo kikuu cha polisi ambapo Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya 
Dar es Salaam, Liberatus Sabas aliwaeleza wanahabari kuwa wanamshikilia 
Zitto kutokana na matamshi aliyoyatoa hivi karibuni kuhusiana na mauaji 
ya askari na raia wilayani Uvinza mkoani Kigoma.
Mpaka
 jana usiku kwa mujibu wa Wakili wake, Jebra Kambole, mwanasiasa huyo 
amenyimwa dhamana na Jeshi la Polisi ambalo limesema kuwa ataendelea 
kushikiliwa kwa ajili ya mahojiano zaidi.






No comments:
Post a Comment