Shirikisho
 la Soka Tanzania (TFF) kupitia Kamati ya Maadili limemfungia maisha 
kutojihusisha na soka aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati yake ya Uchaguzi, Wakili Revocatus Kuuli baada ya kukutwa na hatia ya makosa matatu ya kimaadili.
Mwenyekiti
 wa kamati ya maadili ya TFF, Wakili Hamidu Mbwezeleni alisema Kuuli 
akitambua nafasi yake ndani ya shirikisho hilo, alifanya makosa hayo 
matatu ambayo kimsingi yanastahili adhabu ya kifungo cha maisha 
kujihusisha na masuala ya mpira wa miguu.
Makosa
 matatu ambayo yamemtia hatiani Wakili Kuuli ni kusambaza nyaraka za 
shirikisho kinyume na kanuni na taratibu, kutoa maelezo yanayoonesha 
kuwa na mgongano wa kimaslahi kwa kuwapa watu wasiohusika na pia kufanya
 vitendo vinavyoshusha hadhi ya shirikisho.
"Uamuzi
 huu umechukuliwa kwa kufuata kanuni na taratibu. Hakuna aliyemuonea 
Kuuli niliweke hilo sawa," alisema Wakili Mbwezeleni.






No comments:
Post a Comment