Msemaji Mkuu wa Serikali: Serikali Itaendelea Kutekeleza Miradi Mikubwa Ya Kimkakati

SERIKALI imesema kamwe haitokatishwa tamaa na kauli ya baadhi ya Viongozi na wanasiasa kuhusu dhamira yake ya kutekeleza miradi mikubwa ya kimamkati yenye malengo ya kuleta maguezi ya kijamii na kiuchumi kwa Watanzania.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi wakati wa ziara ya kutembelea Kituo cha Redio ya TBC Taifa na tathmini ya utendaji kazi katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Dkt. Abbasi alisema tangu kuingia madarakani kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Serikali ya Awamu imekuwa ikitekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ambayo wadau mbalimbali wa maendeleo wameipongeza Serikai yake kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa lakini wapo baadhi ya baadhi ya Viongozi na wanasiasa wachache wamekuwa wakipinga mageuzi hayo pasipo na kutoa hoja za msingi.

“Mageuzi yanayoendelea kufanywa hayatakuwa na mwisho, Serikali ya Awamu ya Tano na Watendaji wote tunaomsaidia Rais John Pombe Magufuli tumedhamiria kuleta mapinduzi ya kweli kwa kuboresha huduma za msingi kwa wananchi na tutapokea maoni na ushauri lakini kamwe haturudishwi nyuma na Viongozi na watendaji wanaopinga mageuzi haya” alisema Dkt. Abbasi.

Akitolea mfano Dkt. Abbasi alisema mara baada ya Serikali kutangaza dhamira ya kuanzisha mradi wa kihistoria wa kufua umeme wa Stiegler’s Gorge uliopo Wilayani Rufiji mkoani Pwani wapo baadhi ya wanasiasa na Viongozi wamekuwa wakipinga mradi huo kwa kigezo cha uharibifu wa mazingira ya eneo hilo, jambo ambalo lililenga kupeleka taswira hasi kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo.

Anasema mageuzi mengine yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ni pamoja na ujenzi wa ukuta katika machimbo ya madini ya Tanzanite, ambapo kutokana na hatua hizo katika kipindi cha mwezi Julai hadi Novemba Serikali imeweza kukusanya mapato ya kiasi cha Tsh Milioni 890.

Kwa mujibu wa Dkt. Abbasi alisema katika kuelekea katika mageuzi ya kijamii na kiuchumi, Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na kuweka mfumo imara wa usimamizi wa fedha za umma ikiwemo makusanyo ya kodi, hatua inayoiwezesha Serikali kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli itaendelea kutekeleza sera na programu mbalimbali ikiwemo sera ya elimu bure katika ngazi za elimu ya awali, msingi na sekondari, ambapo Serikali imekuwa ikitoa Tsh Bilioni 23 kila mwezi kwa ajili ya gharama za uendeshaji wake.

Akifafanua zaidi alisema kutokana na kuongezeka kwa kiwango cha ukusanyaji wa kodi, Serikali imeweza kufanya mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali za kijamii ikihusisha afya, maji, barabara pamoja na ununuzi wa ndege mpya nne za Serikali na hivyo kufufua upya huduma za Shirika la ndege Nchini (ATCL) ambazo zilisimama kwa kipindi kirefu.

Akianisha mafanikio ya ATCL, Dkt. Abbasi anasema moja ya mageuzi makubwa yaliyofikiwa kwa sasa na shirika hilo ni pamoja na ongezeko la abiria kutoka abiria 3000-4000 kwa mwezi ambapo kwa sasa wateja wanaotumia Ndege za Shirika hilo wamefikia 30,000 kwa mwezi.

“Mpaka sasa tuna ndege nne za Serikali, na mwezi Desemba tutapokea ndege nyingine 2 aina ya Airbus na mwakani (2019) mwezi Oktoba tutapokea ndege nyingine 1 na kuzifanya ndege mpya za Serikali kufikia saba, na hivyo kufanya sekta ya uchukuzi kuwa katika mabadiliko makubwa ya utendaji na uendeshaji” alisema Dkt. Abbasi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive