SERIKALI
 imesema kamwe haitokatishwa tamaa na kauli ya baadhi ya Viongozi na 
wanasiasa kuhusu dhamira yake ya kutekeleza miradi mikubwa ya kimamkati 
yenye malengo ya kuleta maguezi ya kijamii na kiuchumi kwa Watanzania.
Hayo
 yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Idara ya Habari 
(MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi wakati wa 
ziara ya kutembelea Kituo cha Redio ya TBC Taifa na tathmini ya utendaji
 kazi katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano.
Dkt.
 Abbasi alisema tangu kuingia madarakani kwa Rais Dkt. John Pombe 
Magufuli, Serikali ya Awamu imekuwa ikitekeleza miradi mikubwa ya 
maendeleo ambayo wadau mbalimbali wa maendeleo wameipongeza Serikai yake
 kwa mafanikio makubwa yaliyofikiwa lakini wapo baadhi ya baadhi ya 
Viongozi na wanasiasa wachache wamekuwa wakipinga mageuzi hayo pasipo na
 kutoa hoja za msingi.
“Mageuzi
 yanayoendelea kufanywa hayatakuwa na mwisho, Serikali ya Awamu ya Tano 
na Watendaji wote tunaomsaidia Rais John Pombe Magufuli tumedhamiria 
kuleta mapinduzi ya kweli kwa kuboresha huduma za msingi kwa wananchi na
 tutapokea maoni na ushauri lakini kamwe haturudishwi nyuma na Viongozi 
na watendaji wanaopinga mageuzi haya” alisema Dkt. Abbasi.
Akitolea
 mfano Dkt. Abbasi alisema mara baada ya Serikali kutangaza dhamira ya 
kuanzisha mradi wa kihistoria wa kufua umeme wa Stiegler’s Gorge uliopo 
Wilayani Rufiji mkoani Pwani wapo baadhi ya wanasiasa na Viongozi 
wamekuwa wakipinga mradi huo kwa kigezo cha uharibifu wa mazingira ya 
eneo hilo, jambo ambalo lililenga kupeleka taswira hasi kwa wananchi na 
wadau mbalimbali wa maendeleo.
Anasema
 mageuzi mengine yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ni pamoja na 
ujenzi wa ukuta katika machimbo ya madini ya Tanzanite, ambapo kutokana 
na hatua hizo katika kipindi cha mwezi Julai hadi Novemba Serikali 
imeweza kukusanya mapato ya kiasi cha Tsh Milioni 890.
Kwa
 mujibu wa Dkt. Abbasi alisema katika kuelekea katika mageuzi ya kijamii
 na kiuchumi, Serikali ya Awamu ya Tano imeendelea kuungwa mkono na 
wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na kuweka mfumo imara wa usimamizi 
wa fedha za umma ikiwemo makusanyo ya kodi, hatua inayoiwezesha Serikali
 kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Aliongeza
 kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe 
Magufuli itaendelea kutekeleza sera na programu mbalimbali ikiwemo sera 
ya elimu bure katika ngazi za elimu ya awali, msingi na sekondari, 
ambapo Serikali imekuwa ikitoa Tsh Bilioni 23 kila mwezi kwa ajili ya 
gharama za uendeshaji wake.
Akifafanua
 zaidi alisema kutokana na kuongezeka kwa kiwango cha ukusanyaji wa 
kodi, Serikali imeweza kufanya mageuzi makubwa katika sekta mbalimbali 
za kijamii ikihusisha afya, maji, barabara pamoja na ununuzi wa ndege 
mpya nne za Serikali na hivyo kufufua upya huduma za Shirika la ndege 
Nchini (ATCL) ambazo zilisimama kwa kipindi kirefu.
Akianisha
 mafanikio ya ATCL, Dkt. Abbasi anasema moja ya mageuzi makubwa 
yaliyofikiwa kwa sasa na shirika hilo ni pamoja na ongezeko la abiria 
kutoka abiria 3000-4000 kwa mwezi ambapo kwa sasa wateja wanaotumia 
Ndege za Shirika hilo wamefikia 30,000 kwa mwezi.
“Mpaka
 sasa tuna ndege nne za Serikali, na mwezi Desemba tutapokea ndege 
nyingine 2 aina ya Airbus na mwakani (2019) mwezi Oktoba tutapokea ndege
 nyingine 1 na kuzifanya ndege mpya za Serikali kufikia saba, na hivyo 
kufanya sekta ya uchukuzi kuwa katika mabadiliko makubwa ya utendaji na 
uendeshaji” alisema Dkt. Abbasi.






No comments:
Post a Comment