Aliyekuwa
 mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kisangura wilayani Serengeti, Mkoa wa 
Mara, Emmanuel Nyakitare, (15), amefariki baada ya kukatwa mguu kwa 
panga na mwanafunzi mwenzake wakiwa wanachunga ng’ombe.
Emmanuel
 alifariki wakati akisubiri matokeo ya mtihani wa darasa la saba, 
yaliyotangazwa hivi karibuni. Chanzo cha tukio ni kugombania eneo la 
kulisha mifugo baada ya mtuhumiwa, Charles Kaheke (13), mwanafunzi wa 
darasa la sita katika Shule ya Msingi Kisangura kumkata kwa panga 
marehemu kwa kumtuhumu kulisha mifugo eneo lisilo lake.
Ofisa
 Tarafa ya Rogoro, Gasper Richard, alisema tukio hilo lilitokea Oktoba 
29, mwaka huu, baada ya wanafunzi hao kugombana na baada ya kutenda kosa
 hilo mtuhumiwa alikwenda shuleni bila mfuko wa madaftari kama ilivyo 
kawaida, mwalimu wake alipomuuliza kwa nini hakuwa na daftari akamjibu 
mwalimu kwamba amnunulie ampe.
“Siku
 ya tukio marehemu alikwenda kuchunga mifugo yao eneo hilo jirani na 
nyumbani kwa akina Kaheke, (mtuhumiwa) ambaye alipotoka shule kuja 
kupata chakula cha mchana alimkuta marehemu eneo hilo, katika kuzozana 
ndipo mmoja alimkata mwenzake kwa panga na kuvuja damu nyingi,” alisema.
Akielezea
 tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu, alisema lilitokea
 Oktoba 29, mwaka huu, kati ya saa 6 na saa 7 mchana, wakati wanafunzi 
hao wakichunga mifugo, ndipo ulipozuka ugomvi kugombania eneo la 
malisho, ndipo mtuhumiwa alikasirika na kumkata mguu mwenzake kwa panga,
 hivyo kuvuja damu nyingi na kusababisha kifo chake.
“Hata
 hivyo, baada ya kuona amesababisha kifo cha mwenzake alitokomea na 
kukimbia kwenda kusikojulikana na mpaka sasa haijulikani alipo na 
marehemu Nyakitare alikuwa akisubiri matokeo ya darasa la saba mwaka 
huu, baada ya kufanya mtihani,” alisema Babu.
Babu,
 ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya 
Serengeti, alisema baadaye wazazi wa mtuhumiwa walikwenda kwa familia ya
 marehemu na kuomba msamaha na kuahidiana mambo ambayo hayakuwekwa wazi,
 hivyo kulimaliza suala hilo bila kufika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa 
hatua zaidi.






No comments:
Post a Comment