Wabunge
 wasumbufu wanapokuwa ndani ya ukumbi wa Bunge, wamepatiwa mwarobaini 
baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kusema anaweza kuwaona wabunge wote
 ukumbinu kupitia kwenye kifaa maalumu kilichofungwa kwenye meza yake.
Ndugai alisema hayo bungeni   Dodoma jana alipokuwa akiendesha kikao cha 13 cha Bunge la 11.
Wakati
 Waziri Kivuli wa Fedha, Halima Mdee akiwasilisha maoni ya Kambi Rasmi 
ya Upinzani bungeni juu ya Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa 
na Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2019/20, Ndugai 
alionekana kukemea wabunge waliokuwa wakipiga makofi kwa kutumia vitabu.
“Waheshimiwa
 wabunge siyo busara kutumia vitabu kupiga makofi, halafu mnatumia 
kitabu chenu (cha hotuba ya kambi ya upinzani) hiki.
“Siyo vizuri tumieni mikono, nawaona wote uipitia hiki kifaa hapa,” alisema Ndugai.
Pia katika kikao hicho cha asubuhi, kuna wakati wabunge walikuwa wakipiga kelele huku shughuli zikiendelea.
Spika
 Ndugai aliwakemea akitaja upande (wa upinzani au CCM) wenye kelele 
zaidi huku akisisitiza kuwa alikuwa anawaona wabunge hao kupitia kifaa 
hicho.
Kifaa
 hicho kipo kwenye kiti ambacho Spika ama mtu mwingine anayeongoza kikao
 cha Bunge huketi wakati Bunge likiendelea na kikao cha kawaida.
Kifaa
 hicho pia kipo eneo la makatibu wa Bunge ambako wakati Bunge likiwa 
limekaa kama kamati, Mwenyekiti anayeongoza kikao hicho huketi eneo 
hilo.
Jana,
 Ndugai alitoa kauli hiyo wakati Bunge likiwa limekaa kusikiliza Waziri 
wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango, akiwasilisha Mpango wa Maendeleo 
ya Taifa na lilipokaa kama kamati ya mipango kusikiliza hotua ya Kamati 
ya Bajeti ya ile ya Kambi ya Upinzani.
Ndugai
 akiwa ameketi kama Spika na hata alipoketi kama mwenyekiti wa kamati ya
 mipango, alionekana akiwakemea wabunge kwa nyakati tofauti huku akisema
 alikuwa anawaona kupitia teknolojia hiyo.
Teknolojia
 hiyo, mbali na kusaidia kuona wabunge wasumbufu pia itasaidia kuona 
haraka   Mbunge anayetaka kuuliza swali au kutoa hoja yoyote.






No comments:
Post a Comment