Kamishna
 wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake
 wawili wanaokabiliwa na kesi ya kutakatisha fedha wanaendelea kusota 
rumande kutokana na upelelezi wa kesi yao kutokamilika.
Mbali
 na Kitilya ambaye pia Mwenyekiti wa Kampuni inayoshughulikia Uwekezaji 
wa Mitaji na Dhamana (Egma), washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni 
aliyekuwa Miss Tanzania (1996), Shose Sinare na Ofisa wa Benki ya 
Stanbic, Sioi Solomon.
Kesi
 hiyo imetajwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya 
Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambapo upande wa Jamhuri ulidai 
upelelezi haujakamilika huku Wakili wa Serikali Mwandamizi, Mutalemwa 
Kishenyi akidai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa upelelezi wake 
haujakamilika  na kwamba wanaelekea ukingoni kukamilisha.
Akijibu Wakili wa utetezi Alex Mgongolwa alihoji ni ukingo gani huo ambao unazungumziwa na upande wa mashtaka.
Hakimu
 Shaidi aliutaka upande wa mashtaka kufanya jitihada za kukamilisha 
upelelezi wa kesi hiyo ili hatma ya washtakiwa hao ijulikane na 
kuahirisha kesi hiyo hadi Novemba 30, mwaka huu na kuutaka upande wa 
mashtaka kufanya jitihada kukamilisha upelelezi.
Washtakiwa
 hao kwa pamoja  wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha
 kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha ambapo Machi 2013 jijini 
Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani milioni sita, wakionyesha 
kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa 
mkopo  na zililipwa kupitia  Kampuni ya Egma T Ltd.






No comments:
Post a Comment