Bodi ya Nyama Tanzania imetoa tahadhari kwa wananchi na kuwataka kuacha kula nyama inayouzwa ikiwa imewekwa kwenye ndoo au kupangwa kwenye meza za mabucha kwa sababu si salama kwa afya.
Vilevile
 imewataka wauza nyama kwenye mabucha kuacha kukata nyama kwa kutumia 
magogo kwa vile    wanahatarisha usalama wa walaji.
Akizungumza
 na waandishi wa habari   Dar es Salaam jana, Ofisa Nyama wa Bodi hiyo, 
Edgar Mbio, alisema  nyama hiyo na ile inayokaa buchani zaidi ya saa 
nne.
Mbio alisema kwa utaalamu nyama kama hiyo inakosa sifa ya kuwa na ubora unaofaa kwa matumizi ya binadamu.
“Biashara ya mifugo hufanyika machinjioni na buchani, hatutegemei kuona kinyume na hapo.
“Watu
 wanaonunua nyama kwenye meza… ndoo hizi ndizo zinazoleta madhara kwa 
sababu hazijakaguliwa, pia wale wanaonunua nyama ambayo imeshinda 
inanig’inia buchani nayo inakuwa imeshapoteza ubora kwa kuwa kwa kawaida
 nyama inapaswa kuhifadhiwa si zadi ya saa nane,” alisema Mbio.
Alisema
 wapo pia ambao hununua nyama katika  bucha  ambayo wanatumia vibao 
kukatia navyo si salama kwa sababu muuzaji anapokata anaacha ubora wa 
kitoweo hicho kwenye kibao.
Alisema
 mtu yeyote anayekula nyama iliyochinjwa na kuhifahiwa holela lazima 
apate madhara  kwa kuwa inakuwa si bora na salama hivyo haifai kwa 
matumizi ya binadamu.
Ofisa
 huyo alisema bodi ya nyama inaamini nyama bora na salama inaanzia kwa 
mfugaji kwa kufauta kanuni za ufugaji bora  zinazofuata taratibu ikiwamo
 kuuza  ng’ombe wa umri  chini ya miaka kumi.
Awali,
 Kaimu Msajili wa Bodi hiyo,  Imani Sichalwe aliwataka wananchi kuongeza
 kasi ya kula  nyama ili kufikia kilo 50 kwa mwaka  kwa kila mmoja.
Mbio alisema hicho  ndicho kiwango kilichopendekezwa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO).
Alisema
 takwimu zinaonyesha kila mwananchi nchini kwa kwa sasa anakula kilo 15 
tu ya nyama  kwa mwaka hivyo   kuwa  na tofauti ya kiko 35  kwa kila 
mlaji.
“Tunakula nyama kwa kiwango cha chini ikilinganishwa  na  mahitaji yanayopaswa  ndani ya miili yetu.
“Pamoja na hali ya uzalishaji wa nyama nchini kuwa juu lakini bado watu hawali nyama,” alisema Sichalwe.
Alisema
 uchunguzi uliofanywa na bodi umebaini hali hiyo inatokana na bidhaa 
hiyo kuuzwa kwa bei ghali ambayo kwa wastani huuzwa kuanzia Sh 6,000 
hadi Sh 15,000 kwa kilo moja.
Alisema
 ili kuboresha ulaji wa nyama bodi  imeanza kuhamasisha utumiaji wa 
mizani za digitali ambao utamuwezesha mlaji kununua kulingana na uwezo.
“Hii
 mizani itawaisaidia wananchi ambao wanahitaji kula nyama lakini  hawana
 fedha za kununua  kwa bei ya kiwango cha mizani iliyopo sasa.
“Mfano
 mwenye bucha akiwa na mzani wa digitali anaweza kumuuzia mlaji nyama 
hata ya Sh 500, tunaamini tutaongeza idadi ya walaji kwa njia hii,” 
alisema Sichalwe.
Alisema  kwa mujibu wa bajeti ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi,   Tanzania ni nchi ya pili  ikifuatiwa na Ethiopiakwa mifugo mingi.
Kwa
 sasa nchi  ina   ng’ombe wapatao  milioni 30.5, mbuzi milioni 18.8, 
kondoo milioni 5.3, kuku wa asili milioni 38.2, kuku wa kisasa milioni 
36.6, nguruwe milioni 1.9  na punda 595,160.
Alisema
 bajeti hiyo imeonyesha pia  uzalishaji nyama nchini   mwaka 2017/18  
ulikuwa  tani 679,992  za nyama ya ng’ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe.
“Kati
 ya  tani 2,608.93 za nyama, tani 1,030.78 ni za ng’ombe, tani 1,248.14 
mbuzi, kondoo tani 50.00 na punda tani 280.00 ziliuzwa nje ya nchi,” 
alisema Sichalwe.
Alisema  
 tani 1,224.55 za nyama  ikiwamo nguruwe tani 506.05, ng’ombe tani 
711.03 na kondoo tani 7.47 ziliingizwa ndani ya nchini.






No comments:
Post a Comment