Jeshi
 la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam limefanikiwa kukamata silaha moja 
aina ya Short Gun, risasi nne za short gun na mlipuko moja 
uliotengenezwa kienyeji.
Kaimu
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, LIBERATUS SABAS-DCP 
ametoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari leo Jijini Dar es 
Salaam, amesema Silaha hiyo ilikamatwa tarehe 25 Oktoba 2018 majira ya 
saa 21:30 huko maeneo ya Kijichi. Askari wakiwa doria waliitilia mashaka
 pikipiki iliyokuwa haina namba za usajili ikiendeshwa na kijana mmoja 
akiwa amewapakia wenzake wawili.
Vijana
 hao baada ya kutambua kuwa wanafuatiliwa na Polisi walianza 
kuwafyatulia risasi huku wakikimbia, ndipo askari walipojibu mapigo na 
kufanikiwa kumjeruhi kijana mmoja na kupelekea kufariki akiwa anapelekwa
 hospitali.
Kijana
 huyo alipekuliwa na kukutwa akiwa na silaha aina ya Shotgun iliyokatwa 
mtutu na kitako ikiwa na risasi nne pamoja na mlipuko mmoja.
Msako
 mkali unaendelea kuwasaka watuhumiwa wote waliotoroka ikiwa ni pamoja 
na wahalifu wengine wanaofanya matukio ya kihalifu kwa kutumia silaha za
 moto ndani ya jiji la Dar es Salaam.
Katika
 tukio lingine, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam huko 
maeneo ya Kijichi limefanikiwa kukamata silaha ndogo bastola aina ya 
Star ambayo haikuwa na namba za usajili na risasi nne ndani ya magazine.
Katika
 tukio hilo lililotokea tarehe 1 Novemba 2018 majira ya saa 22:15 huko 
maeneo ya Kijichi Mgeninani askari wakiwa doria walitilia mashaka 
waendesha pikipiki yenye usajili wa namba MC 854 BBY aina ya TVS 
iliyokuwa ikiendeshwa na mtu mmoja huku akiwa amepakia watu wengine 
wawili. 
Askari
 walipowasimamisha watu hao walikataa kutii amri halali na ghafla watu 
hao walifyatua risasi hewani ndipo Polisi walijibu mapigo na kuwajeruhi 
majambazi hao ambao walifariki wakiwa wanapatiwa matibabu hospitalini. 
Watu hao walipekuliwa na kukutwa na silaha hiyo.
Kukamatwa kwa mtandandao wa wizi wa magari
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watuhumiwa 14 kwa tuhuma za wizi wa magari.
Watuhumiwa
 hao wamekamatwa sehemu mbalimbali hapa jijini Dar es Salaam na mikoa 
mingine wakiwa na magari 7, Bajaji moja na pikipiki moja ya wizi vyote 
vimeibwa maeno mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam.
Watuhumiwa
 hao ni Luckman Ramadhani (36 , Ignasi Faustine (35), Ally Shaweji (30),
 Stephen Mwanzalima (43), Emmanuel Mabula (42), Dismas Mfoyi (32), 
Nyamuhanga Matiko (29), Freeman Paul (35), Ayubu Makame (41), Erasto 
Nyamboneke (35), Seleman Saidi (42), Dickson Mbembaji (32), Ally Rashidi
 (35) na Robert Nassoro (46)
Magari
 yaliyokamatwa ni T 162 BLW Toyota land Cruiser MALI YA UWT-TANZANIA, 
STL 6434 Toyota Land Cruise MALI YA WIZARA YA AFYA, T 855 DLE Toyota 
Harrier, T 199 DEU Toyota Noah, T 249 DLL Toyota IST, T 255 AJG Rav4 
gari hii ILIIBIWA udsm IKIWA na namba T 271 DFF, T 556 DJQ Toyota Allion
 ,  MC 854 BYY pikipiki aina ya  TVS Honda , MC 639 BYA Bajaji
Aidha
 kuna magari zaidi ya manne ambayo yamekamatwa mikoani, na yako njiani 
yanaletwa hapa jijini Dar es salaam kwa ajili ya uchunguzi na utambuzi.
Watuhumiwa
 wanahojiwa na watafikishwa mahamani kwa hatua zaidi. Jeshi la polisi 
linaendelea na msako mkali dhidi ya wezi wa magari na watuhumiwa 
wengine.






No comments:
Post a Comment