Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, January Makamba amesema kuwa mgogoro wa kiwanda cha Chai cha Mponde ulitaka kumfanya achukuwe uamuzi wa kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi kisiasa na kiserikali.
Hatua
 hiyo ilitokana na namna ambavyo viongozi wenzake walivyokuwa 
wamegawanyika katika namna ambavyo usuluhisho wa mgogoro huo ulivyokuwa 
ukionekana kutaka kuwanyima haki wananchi.
Waziri
 huyo alizungumza hayo jana Novemba 1 kwenye mkutano wa hadhara 
uliofanyika katika kata ya Mponde wilayani Bumbuli wakati wa ziara ya 
Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa hapo juzi.
Alisema
 alishadhamiria kuachana na nyadhifa zake baada ya kuona viongozi 
wenzake walitofautiana katika swala hilo wakidhani anamaslai nalo.
“Niliona
 ni wajibu wangu kusimamia haki za wananchi na maslahi yao hata kama 
ningetengwa na kunyanyaswa kwani naamini siku zote yule anayesimamia 
haki Mwenyezi Mungu hawezi kumtupa” alisema Waziri Makamba.
Amesema
 mgogoro huo ulileta mpasuko kwa viongozi wa ngazi ya mkoa hadi shina 
lakini imani yake kwa sasa ni kwamba wameelewa alichokuwa akikitetea na 
sasa wapo pamoja.
“Wananchi
 na Wakulima wa chai wameumua wamenyanyasika sana, wamedhulimiwa lakini 
siasa ninaimani kwa mikakati ya serikali sasa uchumi utaimarika” alisema
 Waziri huyo.
Hata
 hivyo aliiomba serikali kuwasaidia wakulima kufufua zao hilo kwa 
kuwapatia miche bora, pembejeo za kilimo ili kufufua zao hilo.
Katika
 hatua nyingine Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa alisema kuwa 
serikali imekichukuwa kiwanda hicho na sasa wapo kwenye maandalizi ya 
kukifufua upya.
Alisema
 kwa sasa wanafanya uhakiki wa madeni yote pamoja na ukaguzi wa mashine 
na mitambo katika kiwanda hicho ili kujiridhisha kabla hakijaanza 
kufanyakazi tena.
Alisema
 tayari deni la kiwanda ni sh Bil 4.4 na kwa sasa anataka afahamu madeni
 yote mpaka ya wafanyakazi wa kiwanda hicho ili baada ya hapo wajipange 
kwa ajili ya ulipaji wa  madeni hayo ili kiwanda kianze upya.
Katika
 hatua hiyo Waziri Mkuu amemuagiza meneja wa kiwanda hicho, Stephen 
Wahome kuhakiki idadi ya wafanyakazi waliokuwepo awali kiwandani hapo 
kujua madai yao ya pamoja na idadi ya vifaa vilivyokuwepo kiwandani 
hapo.
“Watu
 wote waliokuwa wakidai kiwanda hiki serikali italipa madeni yao wakati 
tukiendelea na jitihada za kukifufua kiwanda hiki kiweze kurudi katika 
hali yake ya uzalishani na wananchi waweze kunufaika” alisema Waziri 
huyo.
Waziri
 Majaliwa alisema kuwa mgogoro wa kiwanda hicho ulianza Mara baada ya 
wakulima kuanzisha Umoja wa wakulima wa chai UTEGA na kuusajili kama 
Shirika la kijamii NGOs badala ya chama cha ushirika.
Alisema kuwa chama hicho kiliwabagua wakulima na kutoa upendeleo kwa baadhi ya wakulima hali iliyosababisha mgogoro huo.
Alisema
 kuwa mgogoro ulikuwa zaidi baada ya viongozi wa UTEGA nao kugeukana na 
kuuza kiwanda kwa mwekezaji bila ya kutoa taarifa kwa wakulima wala 
wanachama wao.
Hivyo
 kutokana na kasoro hizo huku maslahi ya mkulima yakiwa madogo ndipo 
serikali ilipoamua kuchukuwa kiwanda chake ili iweze kukiendesha 
mwenyewe kwa maslahi ya wakulima na wananchi.






No comments:
Post a Comment