Spika wa Bunge, Job Ndugai amemzuia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kujibu swali juu ya kuitwa nchini kwake balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Roeland van de Geer kwa kile alichokisema swali hilo lilikuwa nje ya uwezo wa Serikali.
Swali
 hilo liliwasilishwa bungeni na Mbunge Cecil Mwambe wakati wa kipindi 
cha maswali na majibu kwa Waziri Mkuu ambapo alihoji juu ya wito wa 
balozi huyo wa Umoja wa Ulaya.
“Hivi
 karibuni tulishuhudia balozi wa EU alikuwa ameitwa kwao kujadili 
mahusiano ya nchi yetu na jumuiya za kimataifa. Kuna nini 
kinachoendelea?" Alihoji Mbunge Cecil
Akitoa
 maelezo ya maswali hayo Spika Ndugai amesema “Napata wakati mgumu 
kupitisha swali lako sasa kama ameitwa nchini kwao unataka Waziri Mkuu 
ajibu nini, waziri Mkuu tunakushukuru nenda unaweza kwenda kupumzika.”
Ufafanuzi
 wa wito wake ulitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa 
Afrika Mashariki, Balozi Dk.Augustine Mahiga ambapo aliweka wazi kuwa 
balozi huyo hajafukuzwa kama inavyoelezwa bali ameitwa makao makuu ya 
umoja huo.
''Balozi
 wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini Tanzania, Roeland van de Geer 
anayetarajia kuondoka leo (jumamosi iliyopita)  usiku kwenda makao makuu
 ya EU hajafukuzwa bali ameitwa na umoja huo kikazi'', ilieleza taarifa 
ya Waziri Dr.Mahiga.
Taarifa
 za kufukuzwa kwa balozi Roeland van de Geer zilisambaa usiku wa Ijumaa 
mitandaoni na kuzua mijadala mbalimbali, jambo ambalo ilipelekea Waziri 
husika kutolea ufafanuzi.






No comments:
Post a Comment