Mbunge
 wa Mafia, Mbaraka Dau (CCM), amemtuhumu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na 
Mawasiliano, Isaack Kamwele, akidai amekiuka agizo la Waziri Mkuu, 
Kassim Majaliwa, la kupeleka Mafia meli iliyotolewa na mfanyabiashara  
Said Salim Bakhressa akidai ni maagizo ya kisiasa.
Dau
 amesema hayo bungeni jijini Dodoma leo Jumanne Novemba 6, wakati 
akiwasilisha Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Mwongozo wa 
Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Mwaka 2019/20.
Alidai
 kuwa, suala la kupeleka meli hiyo Mafia walilijadili na Waziri Mkuu 
Majaliwa na akakubali ipelekwe Mafia jambo ambalo hata Profesa Makame 
Mbarawa aliyekuwa waziri wa wizara hiyo, aliliridhia.
“Sasa
 hivi nimemfuata na kumkumbusha suala hilo lakini Waziri Kamwele anasema
 ni kauli za kisiasa, sasa inakuwaje waziri anasema agizo la Waziri Mkuu
 ni la kisiasa,” alihoji.
Alisema
 pia alimtuma mbunge mwenzake ili azungumze  na Waziri Kamwele, lakini 
naye alijibiwa kuwa ili meli ipelekwe huko labda nauli iwe Sh 100,000.
Kabla
 ya mchangiaji wa mwisho kusimama, Waziri Kamwele alisimama na kusema; 
“Mbunge wa Mafia amenituhumu kuwa nilitoa maneno yanayoosha nimemdharau 
Waziri Mkuu, sijawahi kusema hayo maneno na waziri mkuu ila nakumbuka 
alinipigia simu akanimbia meli hiyo iliyotolewa na mfanyabiashara 
Bakhresa ifanye safari Mafia, nikatoa maagizo suala hilo liangaliwe kama
 linawezekana nikaambiwa meli hiyo inafanyiwa matengenezo,” amesema 
Kamwelwe akidai kauli ya Dau si nzuri kwa sababu Waziri Mkuu ni bosi 
wake.






No comments:
Post a Comment