Makamu
 wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameagiza uchunguzi ufanyike kwenye ujenzi 
wa madarasa na mabweni ya Shule ya Wasichana Nangwa wilayani Hanang’, 
Manyara kutokana na madai ya kuwapo kwa ubadhirifu wa Sh807 milioni 
unaodaiwa kufanywa na maofisa wa Wizara ya Elimu.
Samia
 alisema hayo jana baada ya kuweka jiwe la msingi la bweni la wasichana 
wa shule hiyo lenye uwezo wa kulaza wanafunzi 160 lililojengwa na 
halmashauri ya wilaya hiyo kwa Sh150 milioni.
Alitoa
 agizo hilo baada ya mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti kusema 
baadhi ya maofisa wa Wizara ya Elimu wanafanya ufisadi kwa kufuja fedha 
za ujenzi wa madarasa na mabweni ya shule hiyo. 
Alisema
 maofisa hao wametumia zaidi ya Sh807 milioni kujenga madarasa na 
mabweni wakati bweni lingine kubwa zaidi limejengwa na halmashauri kwa 
Sh150 milioni.
“Mheshimiwa
 Makamu wa Rais, nataka nikuhakikishie mkoa huu siyo wa majaribio wa 
watu kufuja fedha kwani nikiwaandikia barua wanipe taarifa wanadai jengo
 linajengwa na wizara siyo mkoa,” alisema Mnyeti.
“Kwenye
 Mkoa wa Manyara miradi inasimamiwa kwa ubora ndiyo sababu mwaka huu 
tukashika nafasi ya pili kitaifa kwenye mbio za Mwenge kwa ubora wa 
miradi.”
Aliwapongeza
 mkuu wa Wilaya ya Hanang Joseph Mkirikiti na mkurugenzi mtendaji 
Bryceson Kibassa kwa kusimamia maendeleo. “Hawa ni wasaidizi wangu 
wazuri wanaotimiza wajibu wao ipasavyo,” alisema Mnyeti.
Mama
 Samia ambaye yuko mkoani Manyara kwa ziara ya kikazi, aliagiza 
uchunguzi ufanyike mara moja ili kubaini namna ya fedha hizo 
zilivyotumika katika ujenzi huo.
“Kama
 jengo la bweni kubwa la halmashauri limetumia fedha kidogo na lina 
ubora inakuwaje huku wametumia fedha nyingi namna hivyo? Ni lazima hilo 
lichunguzwe,” alisema.
Pia,
 aliridhia bweni lililojengwa na halmshauri hiyo aliloweka jiwe la 
msingi kuitwa jina lake kisha akaendesha harambee ya kusaidia shule hiyo
 na kupatikana Sh20 milioni.






No comments:
Post a Comment