MC Luvanda Apewa ONYO na Mahakama


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuonya mshereheshaji maarufu nchini Tanzania, Anthony Luvanda maarufu kama MC Luvanda kwa kusafiri bila ya ruhusa ya Mahakama.

Onyo hilo limetolewa leo Jumatatu Novemba 19, 2018 na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi mbele ya mshtakiwa Luvanda, wakili wake Jebra Kambole na wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa.

Hatua hiyo ilifikiwa baada ya wakili Kishenyi kuieleza Mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba mara ya mwisho kulikuwepo na amri ya Mahakama ya kumkamata mshtakiwa huyo kwa kusafiri bila ruhusa ya Mahakama.

Wakili Kishenyi ameeleza Mahakama kwa sababu ametokea akumbushwe masharti ya dhamana.

Baada ya wakili Kishenyi kueleza hayo, wakili wa Luvanda, Jebra Kambole amedai yeye hana pingamizi kuhusu mshtakiwa kukumbushwa masharti ya dhamana na akaomba radhi kwa yaliyotokea na kwamba mambo hayo hayatajirudia tena.

Hakimu Shaidi alimwambia mshtakiwa huyo kila kitu kina nidhamu yake, pia hata katika kesi na kufika mahakamani kuna nidhamu yake.

"Kitendo cha wewe kusafiri bila kuitaarifu Mahakama si kitu kizuri, ukitaka kusafiri toa taarifa."

Hakimu Shaidi ameiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 18, 2018 na akamuonya mshtakiwa huyo afuate utaratibu.

Awali, Hakimu Shaidi Oktoba 23, mwaka huu akitoa  hati ya kukamatwa kwa Luvanda wakati kesi hiyo ilipopangwa kwa ajili ya kutajwa lakini mshtakiwa huyo hakuwepo mahakamani.

MC Luvanda pamoja na kampuni yake, wanakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kutumia kikoa ambacho akijasajiliwa Tanzania.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive