Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuonya mshereheshaji maarufu nchini Tanzania, Anthony Luvanda maarufu kama MC Luvanda kwa kusafiri bila ya ruhusa ya Mahakama.
Onyo
 hilo limetolewa leo Jumatatu Novemba 19, 2018 na Hakimu Mkazi Mkuu, 
Huruma Shaidi mbele ya mshtakiwa Luvanda, wakili wake Jebra Kambole na 
wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa.
Hatua
 hiyo ilifikiwa baada ya wakili Kishenyi kuieleza Mahakama kuwa 
upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba mara ya mwisho 
kulikuwepo na amri ya Mahakama ya kumkamata mshtakiwa huyo kwa kusafiri 
bila ruhusa ya Mahakama.
Wakili Kishenyi ameeleza Mahakama kwa sababu ametokea akumbushwe masharti ya dhamana.
Baada
 ya wakili Kishenyi kueleza hayo, wakili wa Luvanda, Jebra Kambole 
amedai yeye hana pingamizi kuhusu mshtakiwa kukumbushwa masharti ya 
dhamana na akaomba radhi kwa yaliyotokea na kwamba mambo hayo 
hayatajirudia tena.
Hakimu
 Shaidi alimwambia mshtakiwa huyo kila kitu kina nidhamu yake, pia hata 
katika kesi na kufika mahakamani kuna nidhamu yake.
"Kitendo cha wewe kusafiri bila kuitaarifu Mahakama si kitu kizuri, ukitaka kusafiri toa taarifa."
Hakimu Shaidi ameiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 18, 2018 na akamuonya mshtakiwa huyo afuate utaratibu.
Awali,
 Hakimu Shaidi Oktoba 23, mwaka huu akitoa  hati ya kukamatwa kwa 
Luvanda wakati kesi hiyo ilipopangwa kwa ajili ya kutajwa lakini 
mshtakiwa huyo hakuwepo mahakamani.
MC Luvanda pamoja na kampuni yake, wanakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kutumia kikoa ambacho akijasajiliwa Tanzania.






No comments:
Post a Comment