Naibu
 Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye ameitaka 
Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kusitisha mpango wake wa 
kurasimisha bandari bubu zilizopo mkoa wa Dar es Salaam
Hayo
 yameelezwa na Nditiye wakati wa ziara yake Wilayani Bagamoyo ya kukagua
 bandari bubu zilizopo ambapo amebaini uwepo wa bandari bubu zaidi ya 
kumi na tisa zinazosafirisha bidhaa  kwenye eneo la mwambao wa bahari 
lililopo wilayani Bagamoyo. 
Amesema
 kuwa uwepo wa bandari bubu hizo ni kipenyo cha baadhi ya 
wafanyabiashara kukwepa kulipa kodi kwa kutumia bandari rasmi na hivyo 
kupunguza mapato ya Serikali na kuihujumu nchi kwa kufifisha jitihada za
 Serikali za kufikia uchumi wa kati na azma yake ya ujenzi wa viwanda, 
utoaji wa huduma za afya, elimu, maji, umeme na ujenzi wa miudombinu ya 
sehemu mbali mbali nchini
Nditiye
 ameielekeza TPA iache mara moja mpango huo wa kurasimisha bandari bubu 
zilizopo Mbweni na Temeke kwa kuwa Dar es Salaam ipo bandari na itumike 
hiyo kwa shughuli za usafirishaji wa bidhaa na abiria. 
“TPA
 wafute mara moja mpango wao wa kurasimisha bandari bubu za Mbweni, 
Temeke kuwa bandari rasmi wakati kuna bandari ya Dar es Salaam,” amesema
 Nditiye. 
Pia,
 ameongeza kuwa fedha zilizotengwa na TPA kwa ajili ya mpango huo lipewe
 jeshi la bandari ili waweze kununua vifaa kwa ajili ya kufanya doria ya
 kuimarisha ulinzi kwenye mwambao wa bandari
Amefafanua
 kuwa yapo majahazi yanayofanya shughuli za usafirishaji ufukweni mwa 
bahari ya Hindi kwenye mwambao upatao kilomita 300 kwenye eneo la 
Bagamoyo ambapo majahazi yanashusha mizigo kinyemela. 
“Nimeshuhudia
 taratibu za nchi zikikiukwa na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya ya
 Bagamoyo inapata changamoto ila inawadhibiti kwa namna moja au nyingine
 japo yapo majahazi yanayoshusha bidhaa na kuficha kwenye misitu iliyopo
 ndani ya bahari,” amesema Nditiye.
Pia
 ameielekeza Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini (TASAC) kufanya 
utaratibu wa kusajili majahazi yasiyozidi ishirini kwenye eneo la 
Bagamoyo ili yaweze kuwahudumia wananchi wa Bagamoyo na wengine wote 
watumie bandari Dar es Salaam. 
“Yapo
 baadhi ya majahazi yamesajiliwa ila mengine yanafanya shughuli zake 
kinyemela na yanaenda sehemu mbali mbali na baadhi yao wasio waaminifu 
wanatumia vibaya vibali vyao na wanashusha mizigo baina ya saa tano na 
saa tisa usiku,” amesema Nditiye. 
Amefafanua
 kuwa majahazi haya yanakiuka taratibu za nchi kwa kuwawezesha 
wafanyabiashara kukwepa kodi na hivyo kupunguza mapato ya Serikali na 
jitihada za Serikali za kufikia uchumi wa wakati
Naye
 Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Zainabu Kawawa amekiri uwepo wa bandari 
bubu zaidi ya 19 na amemweleza Nditiye kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na 
changamoto za uwepo wa bandari bubu ambazo zinatumia usafiri wa majahazi
 kuvusha bidhaa mbali ili kukwepa ushuru wa mamlaka mbali mbali kwa 
mujibu wa sheria za taasisi husika ambapo wanavusha sukari, mafuta ya 
kula, matairi ya magari, maziwa ya unga, vitenge, khanga, vipodozi na 
wahamiaji haramu ambapo hadi sasa kuna wafungwa wapatao 203 waliopo 
gerezani kutokana na uwepo wa wahamiaji haramu.
Kawawa
 amefafanua kuwa majahazi hayo yanashusha mizigo nyakati za usiku wakiwa
 ndani ya bahari mara nyingine bila kufika ufukweni kwa kufaulisha na 
kupakia kwenye mitumbwi ijulikanayo kwa jina maarufu la ngwanda ili 
iweze kufikishwa nchi kavu kwa ajili ya kusambazwa kwenye maeneo mbali 
mbali ili kukwepa kodi. 






No comments:
Post a Comment