AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA MAUAJI


Na Paulina Juma
KAHAMA.

Mkazi wa kijiji cha Mwabomba Kitongoji cha Bukindwasali Wilayani KAHAMA, YOHANA MASANJA (19 amefikiswa katika mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma ya kumuua LETICIA NDAKI, mkazi wa kijiji hicho cha Mwabomba kinyume na sheria.

Akisoma shitaka hilo mbele ya hakimu wa mahakama hiyo USHINDI SWALLO, mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi, PETER MASAU amesema MASANJA alitenda kosa hilo May 30 mwaka huu saa 5 asubuhi huko Mwabomba Kitongoji cha Bukindwasali wilayani Kahama.

MASAU amesema MASANJA ametenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 196 kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo 2002.

Katika shauri hilo la jinai namba 17/2018 MASANJA hakutakiwa kujibu chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo limeahirishwa hadi June 25 mwaka huu litakapotajwa mahakamani hapo na amerudishwa rumande kwa kuwa kesi hiyo haina dhamana.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels