BAADHI YA WANANCHI WA KAHAMA WATOA MAONI YAO JUU YA BAJETI INAYOENDELEA KUJADILIWA BUNGENI DODOMA

Image result for bajeti ya tanzania 2018/19
Na Leah Samson
KAHAMA.

Baadhi ya wananachi Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA wamesema bajeti ya fedha ya mwaka 2018/2019 inayoendelea kujadiliwa bungeni Mjini Dodoma, huenda ikatoa fursa ya maendeleo kwa wananchi na taifa kutokana na kuwa imegusa maisha ya Watanzania walio wengi.

Wakizungumza na Kahama fm, wananachi hao wamesema wameipokea vizuri bajeti hiyo iliyowasilishwa mwishoni mwa wiki iliyopita na Waziri wa Fedha na Mipaango Dokta PHILIPH MPANGO hasa katika suala la kutokuongeza kodi kwenye bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi.

Katika hatua nyingine wananchi hao pia wametoa wito kwa serikali kuongeza bajeti ya kilimo kwani asilimia kubwa ya wanchi nchini wanategemea sekta hiyo katika kujiimarisha kiuchumi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels