JESHI LA POLISI JIJINI DODOMA LAKAMATA WATUHUMIWA AKIWEMO CHIDI BENZI

Image result for kamanda mkuu dodoma
Na Lilian
DODOMA

Jeshi la polisi Mkoani DODOMA limemtia Mbaroni mtuhumiwa wa kosa la mauji ya mhadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma UDOM pamoja na watuhumiwa wengine 7 akiwemo msanii wa muziki wa bongo fleva RASHID ABDALLAH Maarufu CHID BENZI kwa kosa la kujihusisha na biashara haramu.

Akizungumza na waandisha wa habari kamanda wa polisi mkoani Dodoma GILLES MUROTO Amesema jeshi la polisi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa aliyehusika na mauji ya Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma UDOM ROSE MALFRED MDENYE na mume wake JOHN MWAISAGO yaliyotokea tarehe 25.05.2018 swaswa mtaa wa sulungai na mtuhumiwa huyo kutororka.

Mtuhumiwa huyo ametiwa baroni akiwa mafichoni katika kijiji cha chiwachiwa kata ya mbigu wilaya ya ifakara mkoani Mororgoro na atafikishwa mahakamani kwa kosa la kuua kwa kukusudia.

Kupitia operesheni hiyo ya jeshi la polisi msanii wa mziki wa bongo fleva ABDALLAH RASHID (33) Maarufu kama CHID BENZ amekamatwa akiwa na Bhagi gram 5 katika msokoto ambayo ni kinyume cha sheria na mtuhumiwa huyo atafikishwa tena mahakamani kwa kosa jipya.

Katika hatua nyingine jeshi la polisi limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wengine saba 7 katika maeneo mbalimbali ya nchi ya Tanzania wakijihusisha na biashara haramu ya wanyamapori ambao ni kombe 536 ikiwa ni kinyume cha sheria.

Kwa upande wake afisa wanyamapori mkoa wa Dodoma SLIVANUS OKUDO mewaomba wananchi kufikisha taarifa pindi wanapoona wahujumu wa maliasili na kupeleka nje ya nchi ili hatua kali zichukuliwe dhidi yao.

Jeshi la polisi limewatahadharisha wananchi kuacha kujihusisha na masuala ya uhalifu kwani mkondo wa sheria utafanya kazi yake
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels