CHANGAMOTO YA AFYA, ELIMU VYAWA KERO KWA ALBINO NCHINO


Na Daniel Magwina
KAHAMA.

Imeelezwa kuwa changamoto za Kiafya, Elimu pamoja na Kijamii kuwa ni chanzo kikubwa cha kuendelea kunyanyapaliwa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino), nchini.

Hayo yameelezwa Mjini KAHAMA jana na katibu wa chama cha watu wenye Ualbino (TAS) Wilayani KAHAMA, SITTA GILITU wakati akitoa elimu kwa wanafunzi wa shule ya msingi Nyasubi kuhusu hali ya Ualbino ambapo amesisitiza kuwa mtu mwenye ualbino ni mtu wa kawaida.

SITTA amesema kuwa changamoto zinazowakumba zimeendelea kuwa mwiba kwao na kusababisha baadhi ya wazazi kuwafungia ndani watoto wao wenye ualbino,na kusababisha watoto hao kushidwa kupata elimu na kushiriki shughuli za kijamii na kiuchumi ili kuinua uchumi wa familia zao.

Kwa upande wake mkuu wa shule ya Msingi Nyasubi, ROBISTA ADOLF amekishukuru chama hicho kwa elimu wanayo itoa katika shule mbalimbali na kupiga marufuku kwa mwanafunzi yoyote shuleni hapo kuwaita watu wenye Ualbino majina yasiyofaa.

Ualbino ni hali ya ukosefu wa rangi ya asili katika nywele macho pamoja na ngozi inayowafanya waathirika kushindwa kuhimili mionzi ya jua.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive