HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI WA KAHAMA YAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA WATUMISHI


Na Lilian/Paulina
KAHAMA.

Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa KAHAMA inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa watumishi, malimbikizo ya posho na watumishi kutopandishwa madaraja kwa wakati mambo ambayo yanasababisha kushuka kwa ufanisi miongoni mwa watumishi.

Hayo yamebainishwa katika Risala ya Watumishi wa Hospitali hiyo iliyosomwa na Muuguzi SHARIFA MOHAMED katika maadhimisho ya Siku ya Wauguzi inayoadhimishwa duniani kote Mei 12 ya kila mwaka na ambayo imeadhimishwa leo katika Hospitali hiyo.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Afisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri hiyo, ROBERT KWELA amesema hivi sasa wameanza upanuzi wa hospitali hiyo kwa kujenga jengo la upasuaji na la mama na watoto na kwamba changamoto nyingine zinaendelea kufanyiwa kazi.

Katika maadhimisho hayo ambayo yamebeba kauli mbiu isemayo “WAUGUZI NI SAUTI YA UONGOZI NA AFYA NI HAKI YA BINADAMU”, jumla ya Wauguzi 10 waliostaafu katika hospitali hiyo wametunukiwa vyeti maalum vya kutambua mchango wao katika fani hiyo ya uuguzi.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive