WAKULIMA NA WADAU WA TUMBAKU KAHAMA WASHAURIWA KUJENGA KIWANDA CHA SIGARA HALMASHAURI YA USHETU



Na William Bundala
KAHAMA.
 
Wakulima na wadau wa zao la Tumbaku katika Mkoa wa kitumbaku KAHAMA,Wameshauriwa kujenga kiwanda cha Sigara katika Halmashauri ya USHETU Mkoani SHINYANGA ili kujihakikishia Soko la zao hilo katika siku zijazo.

Wito huo umetolewa na mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, ZAINAB TELLACK wakati wa ufunguzi wa masoko ya Tumbaku uliofanyika katika kata ya Uyogo halmashauri ya Ushetu wilayani KAHAMA.

Bi TELLACK amesema kuwa wakulima wa tumbaku wakiungana wana uwezo mkubwa wa kujenga kiwanda cha Sigara hata cha ukubwa wa kati hatua ambayo amesema itasukuma mbele maendeleo yao binafsi, wilaya ya Kahama na Taifa kwa ujumla.




Sambamba na hayo TELLACK ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya Ushirika kuwa waadilifu na waaminifu katika uongozi wao na kuacha tabia ya wizi wa mali za ushirika na kuwanyanyasa wanachama waliowaweka madarakani.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini, Dkt TITUS KAMANI ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo amewataka wakulima wa Tumbaku na Pamba kudumisha ushirika kwani utawasaidia kuweka nguvu ya pamoja katika kufikia mafanikio.

Awali akimkaribisha Mgeni rasmi Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika Kahama (KACU) EMMANUEL CHEREHANI ameiomba Serikali kufikiria upya kuhusu utaratibu wa kununua Tumbaku kwa fedha za kigeni kwani kununua kwa shilingi ya Tanzania kunasababisha wakulima kupoteza Fedha nyingi.

Mkoa wa kitumbaku Kahama umekuwa wa kwanza kufungua masoko ya zao la Tumbaku Nchini ambapo kwa msimu wa mwaka 2017/2018 jumla ya kilo Milioni 8 na Elfu 11 zitauzwa katika mkoa wa kitumbaku Kahama.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive