AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA WIZI


Na Lilian Katabaro
KAHAMA.

Mkazi wa Kigamboni Jijini DARESALAAM, ABASI JUMA (32) amefkishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya wizi wa kuaminika kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo EVODIA KYARUZI, mwendesha mashitaka wa Polisi EVODIA BAIMO amesema Febuari 15/2013 mtaa wa Malunga, Kahama, JUMA aliiba tani 25 za mchele zenye thamani ya shilingi milioni 50 mali ya PAMBA FESTOS .

BAIMO amesema katika shauri hilo la jinai namba 195/2018 JUMA ametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 27 cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2002.

BAIMO amesema upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na JUMA amerudishwa rumande kwa kukosa dhamana na shauri hilo kutajwa tena Mahakamani hapo June 12 mwaka huu.
Share:

1 comment:

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive