WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA MAUAJI


Na Lilian Katabaro
KAHAMA.

Wakazi wawili wa kijiji cha Ibelansua Wilayani KAHAMA Mkoani SHINYANGA, MARTINE MTOBE (30) na GODFREY JULIUS(29) wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya mauaji.

Mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo IMANI BATENZI, mwendesha mashitaka SAADA ADAM amedai March 23 mwaka huu saa tatu usiku katika kijiji cha Nhendya kata ya Ulowa, Halmashauri ya Ushetu washitakiwa walimuua CHAUSIKU REUBEN kwa kutumia panga.

SAADA amesema Washitakiwa wametenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 196 sura ya 16 kanuni ya adhabu marejeo ya mwaka 2002.

Katika shauri hilo la jinai namba 09/2018, Washitakiwa hawakutakiwa kujibu chochote kwa sababu Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mauaji.

Washitakiwa wamerudishwa rumande na shauri hilo litatajwa tena Mahakamani hapo Mei 5 mwaka huu.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive