AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA YA KUKIUKA MASHARTI YA LESENI YA USAFIRISHAJI


Na Paulina Juma
KAHAMA.

Mkazi wa BUZWAGI Wilayani KAHAMA, PIUS LEONARD (27) amefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya KAHAMA kwa tuhuma ya kukiuka masharti ya leseni ya usafirishaji kinyume cha sheria.

Mbele ya Hakimu mkazi wa Mahakama hiyo IMAN BATENZI, Mwendesha Mashitaka wa jeshi la Polisi, FELIX MBISE amesema LEONARD ametenda kosa hilo Mei 22 mwaka huu katika kituo kikuu cha mabasi cha mjini Kahama.

FELIX amedai kuwa LEONARD akiwa ni wakala wa kampuni ya basi lenye namba za usajili T 997 TZT linalofanya safari zake kati ya Kahama na Dar es Salaam alishindwa kuwasafirisha abiria wake huku akiwa amekwisha wakatia tiketi.

Katika shauri hilo la jinai namba 616 la mwaka huu LEONARD amefanya kosa hilo kinyume na kifungu namba 22 cha kanuni ya leseni ya usafirishaji wa abiria sura ya 317, marejeo ya mwaka 2002.

LEONARD amekana shitaka hilo na yuko nje kwa dhamana na shitaka hilo limeahirishwa hadi June 6 litakapotajwa tena mahakamani hapo.
Share:

No comments:

Post a Comment

IDADI YA WASOMAJI

TUSIKILIZE LIVE KUPITIA TUNEIN

UNGANA NASI FACEBOOK HAPA

10 ZILIZOSOMWA ZAIDI

Labels

Blog Archive