Watu
 wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Manyara  baada ya 
kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya Mirungi  kilo tano sawa na 
mabunda 14 yakisafirishwa kutoka mkoani Arusha kwenda Babati.
Kamanda
 wa polisi mkoa wa Manyara  Agustino Senga  amesema watuhumiwa hao 
wamekamatwa Oktoba 6-2018 Majira ya saa 12 Jioni katika kituo cha 
ukaguzi wa magari  eneo la Minjingu kata ya Nkaiti wilaya ya Babati  
wakiwa wameficha madawa hayo ya kulevya kwenye miili yao maeneo ya 
tumboni hadi mgongoni.
Amewataja
 waliokamatwa ni Aisha Mohamedi  [38] mkazi wa Endasaki, Amani Hassan 
[30] mkazi wa Sakina Arusha ambao walikuwa wakisafirisha Mirungi kilo 
hiyo iliyokuwa imefungwa kwenye  magazeti na kuwekwa  gundi ya karatasi 
na kisha kuifunika kwenye nguo walizokuwa wamevaa.
 Senga
 amesema Watu hao walikamatwa wakiwa katika gari  kampuni ya Makara 
yenye namba za Usajili T 128 -PDC  Fuso wakiwa wamejifunga madawa hayo 
kwa mabunda madogo madogo 14 wakiwa wamejizungushia tumboni ili 
kuonekane ni mtu mwenye vitambi au mwenye ujauzito na muda wowote 
watapandishwa kizimbani.
Ikumbukwe
 kwamba Matumizi ya madawa ya kulevya yameathiri vijana wengi kiafya 
kutokana na baadhi yao kushindwa kufanya kazi , hivyo kulazimika 
kujihusisha na matukio ya wizi katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Kamanda
 amewatahadharisha wakazi wa mkoa wa Manyara na wanaoingia katika mkoa 
huo kwamba Mkoa wake sio mlango wa kupitisha madawa ya kulevya.






No comments:
Post a Comment