MAKAMU
 wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Samia Suluhu amewataka 
wananchi wa Kibaha Mjini Mkoani Pwani ,wajipange kuchagua viongozi 
wepesi kufuatilia maendeleo na kwenda mbio badala ya kuchagua mazezeta 
na mananga ,katika uchaguzi unaokuja wa serikali za mitaa- 2019.
Akihitimisha
 ziara yake ya siku sita mkoani hapo katika mkutano wa hadhara ,Mailmoja
 Samia aliwasihi wasichague watu wazito,wezi na mafisadi bali waweke 
viongozi watakaojenga Kibaha .
“Wanasema
 mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe ,mimi nikija ninaona kasoro zilizopo 
nitakwambieni kuna kasoro lakini warekebishaji ni nyinyi na viongozi 
mtakaowachagua “;:
“Mkichagua
 wazuri wataondosha kasoro zilizopo haraka lakini mkichagua wazito na 
mananga hapa yatazama tuu chini kunyanyuka hayanyanyuki ,kutembea 
hayatembei “alisisitiza Samia .
Akizungumzia
 suala la ardhi anasema”:; Wakati napita ,mheshimiwa mkuu wa mkoa 
alinionyesha eneo kubwa halina kitu chochote nikamwambia mnataka 
manispaa ,lakini mbona eneo hili mwitu mtupu hakuna kuendelezwa 
akaniambia linamilikiwa na taasisi fulani “
Aidha
 ,ameitaka wilaya na halmashauri ya Mji huo kukaa chini na taasisi 
ambazo zimehodhi maeneo bila kuyaendeleza katika kipindi kirefu ili 
ziweze kuingia ubia  .
Awali Mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini ,Silvestry Koka aliomba mji huo upandishwe hadhi na kuwa manispaa kama vigezo vinaruhusu.
Alitaja
 changamoto zinazowakabili kuwa ni ,usambazaji wa maji kwenda kwa 
wananchi unasuasua kasi iongezwe kwani mji unakua ila maji hayajawafikia
 .
”
 Eneo la Tamco-Mapinga zaidi ya miaka mitano wapo wananchi walifanyiwa 
tathmini lakini hawajalipwa fidia zao ,tunaomba utusaidie wananchi hawa 
waweze kufaidika na fidia hizo”alielezea Koka.
Koka
 alitaja tatizo jingine ni ucheleweshaji wa nishati ya umeme , kasi ni 
ndogo kufika kwa baadhi ya maeneo na wawekezaji ,ameomba uwafikie maeneo
 yaliyo katika miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.
Akijibu
 changamoto hiyo, Naibu waziri wa nishati ,Subira Mgalu alisema , 
kupitia serikali ipo sheria iliyoanzisha wakala wa nishati ya umeme 
vijijini lakini maeneo ya miji sheria ile ilikuwa huwezi kufanya miradi 
ya umeme mijini.
“Serikali
 ya awamu ya tano kwa makusudi mazima iliona miji ifaidike na raslimali 
zinazopatikana kwenye mfuko wa umeme vijijini na kwa maelekezo yenu 
tulibuni mradi wa Peri Urban”;alifafanua Subira.
Subira
 alisema ,kiasi cha sh. bilioni 82 zimetengwa kwa ajili ya mradi huo na 
sasa hatua iliyopo ni kumpata mkandarasi ili mradi uanze kazi .
Aliwahakikishia
 wananchi ambao hawana umeme katika kata ya Mailmoja 
,Viziwaziwa,Pichandege ,Pangani, Misugusugu ,Sofu watanufaika na mradi 
huo .
Mwenyekiti
 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ramadhani Maneno, alisema Pwani ipo salama
 na ushindi ni lazima ,iwe jua iwe mvua uchaguzi ujao wa serikali za 
mitaa atahakikisha wanashinda






No comments:
Post a Comment