Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amekabidhi taarifa ya uchunguzi wa mgogoro wa kijiji cha Mabwegere na vijiji saba vya wilaya hiyo na mpango wa utekelezaji wake na kuagiza wote waliohusika kupotosha mipaka ya eneo hilo akiwemo Mkurugenzi Msaidizi wa Upimaji na Ramani wa Wizara ya Ardhi kuchukuliwa hatua za kisheria.
Lukuvi
 alitoa agizo hilo jana mkoani Morogoro wakati akikabidhi taarifa ya 
uchunguzi iliyofanywa na Jaji wa Mahakama Kuu ambaye sasa ni jaji wa 
Mahakama ya Rufaa  Jacob Mwambegele kwa Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dkt 
Kebwe Stephen Kebwe kuhusiana na mgogoro wa mipaka ya kijiji cha 
Mabwegere na vijiji jirani vya Mambegwa,  Mbigiri,  Dumila,  Matongolo 
na Mfulu vilivyopo Wilaya ya Kilosa mkoa wa Morogoro. 
"Wote
 walioshiriki kwa namna moja ama nyingine katika process yote ambayo kwa
 kiasi fulani imeigharimu serikali fedha nyingi na kuipa maumivu 
serikali katika suala hilo ni lazima wachukuliwe hatua kali" alisema 
Lukuvi. 
Taarifa
 ya uchunguzi ilibaini chanzo cha mgogoro ni kukosekana ushirikishwaji 
wa vijiji jirani katika kuainisha na kuweka mipaka ya kijiji cha 
Mabwegere jambo lililosababisha kijiji kiwe na eneo la ukubwa wa hekta 
10, 234 kuliko hata kijiji mama cha Mfulu chenye hekta 1,717 jambo 
lililothibitishwa na ukweli kwamba mipaka ya kijiji hicho imeingia ndani
 ya mipaka ya kata  tatu za Mbigiri,  Msowero,  na Kitete ingawa 
kiutawala kijiji cha Mabwegere kinaratibiwa na  kata ya Kitete. 
Hata
 hivyo,  Waziri wa Ardhi alisema wizara haijakifuta kijiji cha Mabwegere
 bali itaanza kutekeleza mapendekezo ya uchunguzi ya kufuta mipaka ya 
kijiji hicho ambapo sasa TAMISEMI  kwa kushirikiana na wilaya ya Kilosa 
itatakiwa kuanza mchakato wa kuandaa upya mipaka ya vijiji hivyo kwa 
njia shirikishi. 
Katika
 taarifa yake,   Jaji Jacob Mwambegere alipendekeza kwa nia ya kuboresha
 utendaji kazi,  weledi,  maadili na umakini na uwezo wa kulinda na 
kutunza kumbukumbu katika idara ya Upimaji na Ramani na Ofisi ya 
Kamishna wa Ardhi hatua za kinidhamu zichukuliwe ili kuzuia migogoro ya 
ardhi. 
Kwa
 mujibu wa Lukuvi, Wizara ya Ardhi ilikosea katika zoezi la upimaji wa  
kijiji cha Mabwegere lakini wilaya ya Kilosa itakuwa na jukumu la kuanza
 mchakato upya wa uanzishaji wa kijiji hicho. 
Alisema, 
 kwa kuwa serikali inaelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa 
mwakani ni jukumu la Tamisemi kwa kushirikiana na wilaya ya Kilosa 
kuhakikisha mipaka inaandaliwa upya kwa ajili ya kuanzishwa kijiji  
upya. 
Waziri
 wa Ardhi alisisitiza kuwa shughuli za binadamu kama vile ufugaji na 
kilimo hazihusiani na masuala ya mipaka, hivyo wilaya ya Kilosa pamoja 
na kushughulikia suala la mipaka lazima iandae mpango wa matumizi bora 
ya ardhi na kuanza  kupendekeza maeneo ya ufugaji kwa vijiji vyote saba 
na kusisitiza kuwa ni lazima busara itumike katika kushughulikia jambo 
hilo. 
Kwa
 upande wake Naibu Waziri Tamisemi Joseph Kakunda alisema uanzishwaji 
kijiji cha Mabwegere haukufuata sheria na kuwataka wataalamu kuacha kuwa
 na  nidhamu ya woga na kuzingatia kanuni na sheria katika kutekeleza 
majukumu yao. 
Aidha, amemuelekeza Katibu Mkuu TAMISEMI kuunda timu itakayochunguza mchakato mzima wa kuanzisha kijiji hicho, na kila atakaebainika kuhusika na uanzishaji wa kijiji hicho kinyume na sheria achukuliwe hatua.
Aidha, amemuelekeza Katibu Mkuu TAMISEMI kuunda timu itakayochunguza mchakato mzima wa kuanzisha kijiji hicho, na kila atakaebainika kuhusika na uanzishaji wa kijiji hicho kinyume na sheria achukuliwe hatua.
Naye
 naibu Waziri wa Kilimo Merry Mwanjelwa alisisitiza hatua kuchukuliwa 
kwa wote waliohusika na kusema katika serikali hii ya awamu ya tano ni 
lazima kufufua makaburi kwa minajili ya kubaini wote waliohusika 
kuidanganya serikali. 
Taarifa
 ya uchunguzi wa mgogoro wa mipaka kati ya kijiji cha Mabwegere chenye 
jumla ya hekta 10,234 na mifugo takriban 24,146 na vijiji jirani katika 
wilaya ya Kilosa àmbao mara kadhaa ulisababisha vifo vya watu tangu 
mwaka 2008 lifanyika kwa muda wa siku sitini ambapo uchunguzi wake 
ulizingatia uanzishwaji,  upimaji,  utolewaji hati miliki kwa kijiji cha
 Mabwegere,  maeneo yenye mgogoro na hatua zilizokwishachukuliwa juu ya 
mgogoro huo,  uwiano wa ardhi,   mifugo na mahitaji mengine ya ardhi 
pamoja na vyanzo vingine tofauti vya mgogoro.  
Katika
 hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William 
Lukuvi akiambatana na Manaibu waziri Tamisemi Joseph Kakunda na Kilimo 
Merry Mwanjelwa amekutana na viongozi wa Halmashauri za vijiji hivyo 
saba na kuwasomea taarifa ya uchunguzi wa mgogoro wa kijiji cha 
Mabwegere na vijiji jirani. 
Lukuvi
 amewaeleza wananchi hao kuwa ameikubali taarifa nzima ya uchunguzi kwa 
kuwa sheria inampa nafasi ya kuikubali au kuikataa taarifa hiyo, hivyo 
kuikubali kwake ni mwanzo wa utekelezaji wa mapendekezo ya uchunguzi na 
ndiyo maana aliamua kwenda kuwaeleza ukweli wa suala hilo. 
Kwa
 mujibu wa Waziri wa Ardhi viongozi wa wizara nne za Ardhi,  Tamisemi,  
Kilimo pamoja na wizara ya Uvuvi na Mifugo walikaa pamoja na na kupanga 
mpango wa utekelezaji uchunguzi huo na namna ya kushughulikia mgogoro 
baina ya kijiji cha Mabwegere na vijiji jirani. 






No comments:
Post a Comment