JESHI
 la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato 
nchini (TRA) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wamefanikiwa kukamata 
kiwanda  cha kutengeneza Pombe kali ambacho kimekuwa kikizalisha bidhaa 
hiyo bila ya usajili.
Moja ya dira za serikali ya awamu ya tano ni kufikia uchumi wa kati kupitia Viwanda ,hata hivyo baadhi ya wafanyabiahara wanatafsiri Dira hii tofauti kwa kuamua kuanzisha Viwanda bila ya kufuata matakwa ya Sheria na taratibu za nchi.
Hali
 hii imejidhihirisha mkoani Kilimanjaro katika mji mdogo wa Himo baada 
ya Polisi,TRA na TFDA kubaini uwepo wa kiwanda bandia kinachozalisha 
Pombe kali .
Kamanda
 wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamisi 
Issah amesema jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na idara nyingine
 za serikali kuhakikisha kodi ya serikali inapatikana pamoja na kuhakiki
 ubora wa bidhaa kwa ajili ya afya ya watumiaji.
Zoezi
 la kubaini uwepo wa viwanda bandia katka mkoa wa Kilimanjaro ambapo 
katika siku za karibuni viwanda vilivyogundulika ni vile 
vinavyotengeneza Pombe za kienyeji na Pombe kali ,baadhi  vikiwa katika 
wilaya ya Rombo.
 






No comments:
Post a Comment