Kesi 
 ya utakatishaji fedha na kumiliki mali zisizolingana na kipato chake 
halali, inayomkabili aliyekuwa Mhasibu Mkuu wa Takukuru, Godfrey Gugai 
na wenzake wanne, imeshindwa kuendelea kusikilizwa  sababu, Mahakama ya 
Hakimu Mkazi Kisutu haina hela ya kuwaleta mashahidi.
Wakili
 wa Serikali, Pius Hila akisaidiana na wakili kutoka Takukuru, Vitalis 
Peter ameeleza hayo, leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, 
Thomas Simba,  kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa.
Wakili
 Hilla amedai walishaita mashihidi  kutoka nje ya Mkoa wa Dar es Salaam 
lakini wameshindwa kufika kwa kuwa Mtendaji wa Mahakama hakuwa na fungu 
la  fedha, kwa  ajili ya kuwalipa.Ameendela kueleza kwa sasa wamepata  
kibali kutoka kwa  Mtendaji wa Mahakama ambacho kinawaelezea kuwa malipo
 yatasubiri fedha zitakapoingia lakini mashahidi wameshindwa kuja kwa  
gharama zao wenyewe.
"Mheshimiwa
 hakimu kutokana na hali hiyo, tunaomba terehe fupi kwa ajili ya 
kuendelea na usikilizwaji wa kesi hii," ameeleza Hilla.Kutokana na 
maelezo hayo, Wakili wa Utetezi Alex Mgongolwa aliwasilisha maombi 
mawili mahakamani hapo.
,"Mheshimwa,
 tunaomba jitihada za kuwapata mashahidi hao waliopo nje ya mkoa wa Dar 
rs Salaam ziendelee na pia  ni rai yetu kwa  mahakama upande wa mashtaka
 walete mashahidi ambao hawahitaji kuombewa kibali na hawatoki nje ya 
mkoa wa Dar es salaam ili Kesi hii iweze kuendelea," amedai Wakili 
Mgongolwa.
Kutokana
 na hayo, Hakimu Simba amesema, mahakama itazungumza na Mtendaji wa 
Mahakama ili kutafuta fedha sehemu yoyote ili mashahidi hao waweze kuja 
mahakamani na kutoa ushahidi kwa sababu kesi hiyo ni ya muda mrefu.Kesi 
imeahirishwa hadi  Oktoba 15 na 16, mwaka huu kwa ajili ya kuendelea 
kusikilizwa.
Mpaka
 sasa ni shahidi  mmoja wa upande wa mashtaka, Ayoub Akida(52) ambaye ni
 Ofisa Utumishi Mkuu kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa 
(Takukuru), ameshatoa ushahidi wake dhidi ya Gugai.Mbali na Gugai, 
washtakiwa wengine, ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasin Katera.
Katika
 kesi ya msingi, Gugai na mwenzake, wanakabiliwa na makosa 43, kati ya 
hayo 19 ni ya kughushi, 23 ni utakatishaji fedha na moja ni kumiliki 
mali zisizoendana na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika 
maeneo mbali mbali.Gugai anakabiliwa na kosa la kumiliki mali 
zisozoendana na kipato chake, analodaiwa kutenda kati ya January 2005 na
 Decemba 2015.
 Akiwa
 ofisa wa umma ameajiriwa na TAKUKURU alikutwa akimiliki mali za zaidi 
ya Sh. bilioni 3.6 ambazo hazilingani na kipato chake cha awali na cha 
sasa






No comments:
Post a Comment