Waganga 
 wafawidhi wametakiwa   kujadili sababu ya vifo vinavyotokea kwenye 
hospitali zao ili kuzifanyia kazi changamoto hizo na kurudisha taarifa 
Wizara ya Afya.
Hayo
 yamesemwa na Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Wizara ya Afya, 
Dk. Otilia Gowelle, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa waganga wafawidhi 
nchini,  Dodoma jana.
“Waganga
 wafawidhi mnatakiwa kukaa vikao vya utabibu kujadili tiba pamoja na 
kujadili kifo cha kila mgonjwa  kujua changamoto iliyotokea na kuipatia 
ufumbuzi na kuandikia taarifa   kuondokana na vifo hasa vinavyotokana na
 uzazi,” alisema Dk. Gowelle.
Aliwataka
 wataalamu wa tiba kuzingatia vikao vya tiba na kufanyia kazi changamoto
 au maboresho ili kuzitolea taarifa na kuzitatua pamoja na kushirikisha 
wadau wengine.
Dk.
 Gowelle aliwataka pia waganga wafawidhi kuweka mifumo ya ufuatiliaji 
wagonjwa   na kupokea malalamiko  katika hospitali zao   kufanya 
maboresho ya huduma za afya wanazozitoa na kuchukua hatua zinazostahili.
“Kupitia
 kikao hiki, nawataka mkae kama timu na kuandaa mipango kazi ya kuanza 
kushughulikia kwa ukamilifu yale yote yaliyobainika katika taarifa hiyo.
“Lengo ni kuondokana na kero wanazokabiliana nazo wananchi wanapokuja kupata huduma katika hospitali zenu,” alisema Dk. Gowelle.






No comments:
Post a Comment