Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa Kamanda
 wa Polisi wa Mkoa wa Kagera Augustine Ollomi, Kamanda wa Polisi wa 
Wilaya ya Kyerwa Justine Joseph, Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Kyerwa 
Everist Kivuyo na Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Kyerwa Robert Marwa.
Viongozi
 hao wa Polisi wanasimamishwa kazi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za 
kuhusika katika magendo ya zao la kahawa katika Wilaya ya Kyerwa pamoja 
na tuhuma nyingine.
Aidha,Rais
 Magufuli amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 
Mej. Jen Jacob Kingu na Inspekta Generali wa Polisi Simon Sirro 
kuhakikisha uchunguzi wa kina unafanyika na hatua stahiki zinachukuliwa 
endapo watabainika kuhusika katika magendo ya kahawa na makosa mengine 
kwa mujibu wa sheria.
Tuhuma
 dhidi ya viongozi wa polisi katika Wilaya ya Kyerwa zimebainika  wakati
 wa ziara ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim 
Majaliwa Majaliwa.







No comments:
Post a Comment