Vijana
 wanane wa jamii ya wafugaji ya Kimasai (morani) kutoka Kitongoji cha 
Oldonyo Lengai, Kijiji cha Loondolwo, Longido mkoani Arusha, 
wamenusurika kifo baada ya kujeruhiwa na simba.
Kwa
 mujibu wa vijana hao, walikutwa na simba majira ya saa nane alasiri 
juzi kisha kushambuliwa wakati wakichimba kisima kutafuta maji ya 
kunyweshea mifugo.
"Tulijaribu
 kupiga kelele, simba akaanza kutushambulia. Kuona hivyo, wengine wakawa
 wanapiga simu kuomba msaada na kila aliyekuwa anakuja kutoa msaada 
alishambuliwa," alisema Mibaku Mundesyo (35) mmoja wa manusura hao.
Alisema
 walishambuliwa maeneo mbalimbali ya mwili hali iliyosababisha moja wao 
kuwahishwa Hospitali ya Rufani ya Seliani ya jijini hapa kwa matibabu 
zaidi.
Wengine
 walionusurika ni Melubo Sung'are (24) Milya Lemayaka (28), Loning'o 
Sung'are (20), Sakaya Osikarari (20), Ng'ahari ole Bainu (30), 
Leng'arwua Loda (20) na Laari Olchuda (21).
Kwa mujibu wa jamii ya wafugaji ya Kimaasai, morani wana umri wa miaka kuanzia 18 hadi 40.
Mtaalamu
 wa wanyamapori na uwindaji anayemiliki kampuni ya uwindaji ya 
Mantheakis Safaris Ltd, Michel Mantheakis, alisema alimfuatilia simba 
huyo kuchunguza tukio la kujeruhiwa kwa vijana hao, akabaini kwamba 
simba ndiye aliyewashambulia vijana hao.
"Ni kweli simba aliwavamia vijana hao lakini jambo la kushangaza hakuweza kuua mtu zaidi ya kuwajeruhi kwa kucha.
"Nilipomfuatilia
 huyo simba, hakuonekana kuwa na jeraha kwani hata tembea yake haikuwa 
na shida na kama alirushiwa mkuki haukumpata vyema.
"Nimeshangazwa na tukio hili kwani haijawahi kutokea watu wanane kujeruhiwa na simba bila kuwa kwenye uwindaji,” alisema.
Hata hivyo, aliitaka jamii hiyo wakimwona simba wamwache ili sheria zifuatwe.
Mkuu
 wa Wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe, aliyefika katika kitongoji hicho
 na kukutana na wananchi, aliwasihi kuacha kuwinda wanyama kinyume cha 
sheria.
Alisema wanyamapori huingiza fedha nyingi kijiji hapo kutoka kwa kampuni za uwindaji.
Pia
 aliwataka kuwa walinzi wa wanyamapori na akalaani vitendo vya baadhi 
yao kuharibu mitego na kamera zilizowekwa na wawekezaji walioingia nao 
mikataba.






No comments:
Post a Comment